Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Ofisi ya Taifa ya Takwimu yafungua milango

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inapenda kuwajulisha wananchi wote kuwa yeyote anayetaka kuwa Mdadisi au Mkusanyaji taarifa za kitakwimu rasmi katika tafiti mbalimbali zinazoratibiwa na ofisi hii, ni sharti awe amehitimu Mafunzo ya Ukusanyaji Takwimu Rasmi angalau kwa ngazi ya cheti.

Hii ni kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu Na. 9 ya mwaka 2015 inayoipa mamlaka Ofisi ya Taifa ya Takwimu ya kuratibu na kusimamia ukusanyaji takwimu rasmi (official statistics) nchini. 

Hivyo, kuanzia sasa NBS itakuwa inawatumia wadadisi ambao wamehudhuria na kuhitimu angalau cheti cha Ukusanyaji Takwimu katika miradi mbalimbali ili kuboresha zaidi upatikanaji wa takwimu rasmi nchini.

Mafunzo ya Ukusanyaji Takwimu Rasmi yanatolewa na Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika “Eastern Africa Statistical Training Centre” (EASTC) kilichopo Changanyikeni jijini Dar es Salaam.
Kwa mawasiliano zaidi na kujisajili wasiliana na:

Ofisi ya Msajili wa Chuo,
Eastern Africa Statistical Training Centre,
S.L.P 35103,
DAR ES SALAAM.
Barua pepe: info@eastc.ac.tz; 
Tovuti: www.eastc.ac.tz  
Simu namba: 022-2925000 au 0784784106.

Tangazo hili limetolewa na:    
Mkurugenzi Mkuu,
Ofisi ya Taifa ya Takwimu,
DAR ES SALAAM.
05 Oktoba, 2016.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top