Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Taarifa kamili juu ya matokeo Darasa 7 ... Yaone hapa matokeo mapya zaidi

Ufaulu kwa watahiniwa wa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2016 umepanda kwa asilimia 2.52 kutoka asilimia 67.84 mwaka jana hadi asilimia 70.36, huku wavulana waking’ara katika matokeo hayo ambao wengi wametoka shule za Kanda ya Ziwa.
 
Matokeo hayo yaliyotangazwa jana na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dk Charles Msonde ambaye alisema kati ya wanafunzi 10 bora waliofanya vizuri katika mtihani huo, msichana ni mmoja tu, Justina Gerald wa Shule ya Msingi ya Tusiime ya jijini Dar es Salaam.
 
Kati ya wanafunzi hao 10, watahiniwa saba wanatoka Shule ya Msingi Kwema iliyopo mkoani Shinyanga, wawili Tusiime na mmoja kutoka Kaizirege ya Bukoba mkoani Kagera. 

Dk Msonde alisema jumla ya watahiniwa 555,291 kati ya 789,479 waliofanya mtihani huo wamefaulu kwa kupata jumla ya alama 100 na zaidi kati ya alama 250.
 
“Idadi hii ya watahiniwa waliofaulu ni sawa na asilimia 70.36, kati ya hao wasichana ni 283,751 na wavulana 271,540. Mwaka 2015 ufaulu ulikuwa ni asilimia 67.84 kuwapo ongezeko la ufaulu kwa asilimia 2.52,” alisema Dk Msonde.
 
Watahiniwa 16,929 wamepata daraja A, watahiniwa 141,616 wamepata Daraja B, watahiniwa 396,746 wamepata daraja C, watahiniwa 212,072 wakipata daraja D na 21,872 wakipata daraja E . 

Dk Msonde alisema ufaulu katika masomo ya Sayansi na Maarifa ya Jamii umepanda kwa asilimia kati ya 4.06 na 14.76 ikilinganishwa na mwaka 2015 huku masomo ya Kiswahili, Hisabati na Kiingereza ufaulu umeshuka kwa asilimia kati ya 0.39 na 12.51 ukilinganisha na mwaka jana.
 
“Watahiniwa wamefaulu zaidi katika somo la Kiswahili ambalo ufaulu wake ni asilimia 76.81 na somo walilofaulu kwa kiwango cha chini ni Kiingereza lenye ufaulu wa asilimia 36.05,” alifafanua Dk Msonde.
 
Dk Msonde aliwataja watahiniwa waliofanya vizuri na shule zao kwenye mabano kuwa ni:
  • Japhet Stephano, Jamal Athuman na Enock Bundala (Kwema),
  • Justina na Shabani Mavunde (Tusiime),
  • Jacob Wagine, Isaac Isaac, Daniel Kitundu na Benjamin Benevenuto (Kwema)
  •  Azad Ayatullah (Kaizirege).
Wasichana 10 bora:
  1. Justina Gerald (Tusiime)
  2.  Danielle Onditi (Tusiime)
  3. Linda Mtapima (Kaizirege),
  4. Cecilia Kenene (Mugini),
  5. Magdalena Deogratias (Rocken Hill),
  6. Asnath Lemanya (Tusiime),
  7. Fatuma Singili (Rocken Hill),
  8. Ashura Makoba (Kaizirege),
  9. Rachel Ntitu (Fountain of Joy),
  10. Irene Mwijage (Atlas)
Wanafunzi wavulana 10 bora kitaifa,
  1. Japhet Stephano (Kwema),
  2. Jamal Athuman (Kwema),
  3.  Enock Bundala (Kwema),
  4. Shabani Mavunde (Tusiime),
  5. Jacob Wagine (Kwema),
  6. Isaac Isaac (Kwema),
  7. Daniel Kitundu (Kwema),
  8. Benjamin Benevenuto (Kwema),
  9. Azad Ayatullah (Kaizirege)
  10. Benezeth Hango (Kwema).
Shule 10 bora ni:-
  1. Kwema (Shinyanga),
  2. Rocken Hill (Shinyanga),
  3. Mugini (Mwanza),
  4. Fountain of Joy (Dar es Salaam),
  5.  Tusiime (Dar es Salaam),
  6. Mudio Islamic (Kilimanjaro),
  7. Atlas (Dar),
  8. St Achileus (Kagera),
  9. Giftskillfull (Dar),
  10. Carmel (Morogoro).
Shule 10 ambazo hazikufanya vizuri ni:-
  1. Mgata (Morogoro)
  2. Kitengu (Morogoro)
  3. Lumba Chini (Morogoro),
  4. Zege  (Tanga),
  5.  Kikole (Tanga),
  6. Magunga ya Morogoro,
  7. Nchinila (Manyara),
  8. Mwabalebi (Simiyu)
  9. Ilorienito (Arusha)
  10. Chohero (Morogoro)
Mikoa 10 iliyoongoza kitaifa ni Geita, Katavi, Iringa, Dar es Salaam, Kagera, Mwanza, Kilimanjaro, Arusha, Njombe na Tabora wakati Halmashauri 10 bora ni Mpanda Manispaa, Geita Mji, Arusha Mji, Mafinga Mji, Chato, Mwanza Jiji, Moshi Mji, Mji Makambako, Ilemela na Hai.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top