Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CCM yakunjua makucha yake



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekunjua makucha kwa kuwachukulia hatua kali za kinidhamu kwa viongozi na wanachama wake 600, waliobainika kukiuka maadili ya uongozi, ikiwemo kukisaliti Chama katika kipindi cha uchaguzi mkuu uliopita.

Wanachama hao ni kutoka katika mikoa 10 ya Tanzania Bara, ambayo imeshawasilisha ripoti zake makao makuu ya CCM, kuhusu hatua iliyochukua dhidi ya wanachama waliokisaliti wakati wa uchaguzi huo.

Katika orodha hiyo, wapo wanachama waliopewa onyo kali, waliosimamishwa uongozi na wengine kuvuliwa uanachama. Pia wapo wanaosubiri maamuzi ya vikao vya juu kutokana na tuhuma zinazowakabili.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top