Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mama Maria Nyerere amlilia Fidel Castrol


Baada ya Serikali ya CUBA kutangaza kifo cha rais wa zamani wa nchi hiyo FIDER CASTRO kilichotokea leo,mjane wa baba wa taifa mama Maria Nyerere amepokea kwa masikitiko makubwa kifo hicho cha mwanamapinduzi huyo.
Akizungumzia msiba huo mama maria Nyerere amesema CUBA na Dunia nzima ikiwemo Tanzania imepoteza mtu muhimu sana katika mambo ya kupigania haki,usawa na demokrasia.
Amesema wakati wa harakati mwaka wa 1973 Fider Castro alikutana na mwalimu na kujadili mambo mbalimbali kuhusu ukombozi wa bara la afrika pamoja na nchi ambazo hazikuwa huru wakati huo.
Mama Maria Nyerere anampa pole,rais wa nchi hiyo,familia ya hayati Castro pamoja na wananchi wote wa nchi ya Jamhuri ya watu wa CUBA.
Mama Maria Nyerere amesema msiba huo umewagusa si wananchi wa CUBA bali hata watanzania pia umetugusa kutokana na msaada ambao Fider Castro aliutoa kwa nchi yetu kwa kushirikiana na hayati baba wa taifa mwalimu Julius kambarage Nyerere
Kwa upande wake Mbunge wa Afrika Mashariki Charles Makongoro Nyerere naye ameungana na Mama Maria Nyerere kwa kutoa salamu za pole kwa wananchi wan chi hiyo pamoja na kiongozi mkuu wake.
Amewataka wananchi wa CUBa kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu kwa kuwa hayo ni maamuzi ya Mwenyezi Mungu yapaswa kushukuriwa.
Imetolewa na MAKONGORO NYERERE
MBUNGE AFRIKA MASHARIKI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top