Loading...
Achomwa mkuki wa mdomo na kutokezea shingoni
Mtu mmoja Agostino Mtitu mkulima wa kitongoji cha Upangwani kijiji cha Dodoma Isanga amechomwa mkuki mdomoni na umetokezea nyuma ya shingo yake. Amekimbizwa hospitali ya mkoa ili kufanyiwa operesheni ya kuondoa mkuki huo. Ameshambuliwa na wafugaji wa kimasai alipokuwa akimsaidia jirani yake kufukuza Ng'ombe wasiharibu mazao shambani.
Kipande cha mti kinachoonekana mdomoni ndiyo mkuki huo, kimekatwa kupunguza urefu wa mkuki wakati wakimleta hospitali.
Inasemekana MwenyeKiti wa kijiji na MwenyeKiti wa kitongoji hicho nao wamejeruhiwa japo hadi sasa bado hawajafikishwa hapa hospitali
Post a Comment