Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Benki Kuu (BOT) yaelezea juu ya uvumi wa noti ya Tsh. 500

Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuwafahamisha wananchi wote kuwa habari inayoenea katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwamba noti ya shilingi mia tano haitatumika tena baada ya Disemba 31, 2016 sio taarifa ya kweli na ni uvumi unaopaswa kupuuzwa.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Huduma za kibenki BoT, Marcian Kobello ambapo alifafanua kuwa noti ya shilingi 500 itaendelea kuwepo katika mzunguko sambamba na ile sarafu ya shilingi 500 hadi pale noti hiyo itakapotoweka mikononi mwa wananchi.

Aidha, Kobello amewataka wananchi kupuuza taarifa zinazoeleza vinginevyo kwani si za kweli.

Serikali iliamua kuleta sarafu ya TZS 500 baada ya kuwepo malalamiko kuwa noti ya TZS 500 ambayo ndiyo inazunguka zaidi inachakaa mapema sana.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top