Loading...
BREAKING NEWS .... EWURA yatangaza mabadiliko bei ya umeme nchini
*MABADILIKO YA BEI ZA UMEME YALIYOTANGAZWA LEO NA MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA UDHIBITI WA HUDUMA ZA NISHATI NA MAJI (EWURA), FELIX NGAMLAGOSI.*
#Bei za umeme zimepanda kwa 8.5% badala ya 18.19% iliyopendekezwa na TANESCO.
#Ongezeko la bei ya huduma za umeme limetokana na kuzidi kwa gharama za uzalishaji wake.
#Shirika la umeme Zanzibar (ZECO) ambalo linanunua umeme wa jumla kupeleka Zanzibar limeongezewa 5.7% ya bei ya umeme.
#Ongezeko hilo halitaathiri wateja wa majumbani ambao matumizi yao hayazidi uniti 75 kwa mwezi.
#Kundi la TIb linalohusisha viwanda vidogo,mabango na minara ya mawasiliano litakua na tozo ya mwezi ya shilingi 5,520.
#Bei hizo zitaanza kutumika Januari Mosi mwaka 2017.
#TANESCO inatarajia kufanya maboresho ya msongo wa umeme na kutekeleza miradi mipya ya kuunganisha wateja ili kuboresha huduma za umeme.
*IMEANDALIWA NA IDARA YA HABARI (MAELEZO).*
Post a Comment