Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CCM, UKAWA kutikisa nchi kwa siku 30






Dar es Salaam. Baada ya mwaka mzima wa Serikali kuzuia mikutano ya hadhara, vyama vya CCM,  Ukawa, ACT Wazalendo na vingine vinatarajiwa kuwasha moto kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Dimani, Zanzibar na madiwani katika kata 22 kwenye halmashauri 21 za Tanzania Bara kwa mwezi mzima.
Mbali na ubunge, mtifuano huo utafanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Singida, Mwanza, Dodoma, Iringa, Manyara, Mara, Arusha, Katavi, Ruvuma, Kagera, Shinyanga, Kilimanjaro, Simiyu na Pwani.
Uchaguzi huo unatarajiwa fursa ya kwanza kwa vyama vya siasa kupata uwanja wa kufanya mikutano ya hadhara kunadi sera zao na pengine kipimo cha utawala wa Rais John Magufuli katika uongozi wa Serikali na chama tawala.
Mwananchi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top