Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CCM yafanya mabadiliko makubwa ..... Haya ndio yaliyoamuliwa kwenye kikao cha NEC cha leo


TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI
Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imekutana leo tarehe 13/12/2016 jijini Dar es salaam kwa kikao cha siku moja cha kawaida. Kikao hicho kimeongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Dr. John Pombe Magufuli.

Pamoja na mambo mengine, Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imepokea taarifa ya Tathimini ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, baada ya kuitafakari taarifa hiyo, Halmashauri Kuu imeamua yafuatayo;-

1. Kupunguza idadi ya wajumbe wa vikao na idadi ya vikao vya Chama katika ngazi mbalimbali ili kuongeza ufanisi wa utendaji wa Chama na kuongeza muda wa viongozi wa Chama kufanya kazi za Chama kwa Umma badala ya kutumia muda mwingi vikaoni.

Ili kuwa  na vikao vya Chama vyenye tija inapendekezwa kama ifuatavyo:-

a). Halmashauri Kuu ya Taifa kwa sasa ina jumla ya wajumbe 388 idadi ambayo ni kubwa sana, hivyo inapendekezwa idadi hii ipunguzwe na kuwa wajumbe 158 kama  ifuatavyo:-

Wenyeviti wa Mikoa
Mikoa ya Bara 26x1    =   26
Mikoa ya Zanzibar 6x1= 6

Wajumbe wa NEC wa Mikoa
Mikoa ya Bara 26x1=  26
Mikoa ya Zanzibar 6x4= 24

Wajumbe wa NEC wa Taifa
Kutoka  Bara    =    15
Kutoka  Zanzibar  =15

Nafasi za Mwenyekiti = 7


Wajumbe wa NEC wa Jumuiya

UVCCM=     5
UWT=     5
WAZAZI=     5
Wajumbe wa NEC kutoka Bungeni    =5

Katibu wa Kamati ya Wabunge wa CC=1

Wajumbe wa  NEC kutoka BLW =    3

Katibu wa Kamati ya Wawakilishi=    1
         
Wajumbe wa NEC – wanaotokana na Nyadhifa zao
Mwenyekiti wa CCM=    1
- Makamu Mwenyekiti (B)=    1
-Makamu Mwenyekiti (Z)=    1
- Makamu wa Rais =    1
-  Waziri Mkuu        =    1
- Makamu wa Pili wa Rais (Z)    =1
- Spika wa Bunge    =    1
- Spika  wa  BLW    =    1
- Mwenyekiti wa UWT=    1      
- Mwenyekiti wa WAZAZI=1
-Mwenyekiti wa UVCCM    =1
- Katibu Mkuu – WAZAZI    =1
- Katibu Mkuu – UWT =    1
- Katibu Mkuu – UVCCM    =    1
                     Jumla:        158

 
#.Vikao vya kawaida vya Halmashauri Kuu ya Taifa vitafanyika kila baada ya miezi sita badala ya miezi minne kama ilivyo sasa isipokuwa vinaweza kufanyika vikao maalum inapohitajika.

b). Kwa upande wa sasa imeamuliwa wajumbe wa Kamati Kuu wawe 24 badala ya 34 kama ifuatavyo:-

Mwenyekiti wa CCM.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara)
Makamu Mwenyekiti wa CCM    (Zanzibar)
Makamu wa  Rais
Katibu Mkuu wa CCM              
Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara)
Naibu Katibu Mkuu wa CCM  (Zanzibar)
Waziri Mkuu
Makamu wa Pili wa Rais (Z)
Spika wa Bunge la Tanzania
Spika  wa BWL
Mwenyekiti  wa WAZAZI
Mwenyekiti  wa UWT
Mwenyekiti  wa UVCCM
Katibu wa   wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa  Organaizesheni
Katibu wa   wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa  Itikadi na Uenezi
Katibu wa   wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa  Uchumi na Fedha
Katibu wa   wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa  Mambo ya Siasa   na Uhusiano wa Kimataifa  
Wajumbe  watatu (3)  wa kuchaguliwa  na Halmashauri Kuu kutoka Tanzania (B)
Wajumbe watatu  (3) wa kuchaguliwa  na Halmashauri Kuu kutoka Zanzibar

#. Vikao vya kawaida vya Kamati Kuu vipunguzwe ili vifanyike kila baada  ya miezi minne badala ya miezi miwili isipokuwa vinaweza kufanyika vikao maalum inapohitajika.

c). Kwa ngazi ya mkoa, Wajumbe wa Kamati za Siasa za Mikoa wapunguzwe kwa kuondoa wajumbe  watatu ambao ni:-
Katibu wa Uchumi na Fedha wa Mkoa        -    1
Wajumbe wa kuchaguliwa na H/Mkoa    -    2

#. Vikao  vya kawaida vya Kamati ya Siasa ya Mkoa vifanyike kila baada ya miezi mitatu badala ya kila  mwezi kama ilivyo sasa isipokuwa vinaweza kufanyika vikao maalum inapohitajika.

d). Kwa upande wa Wilaya Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya wapunguzwe kwa kuwoandoa:-
Katibu wa Uchumi na Fedha wa Wilaya    -    1
Katibu wa Kamati ya Madiwani            -    1
Wajumbe wa kuchaguliwa na H/Kuu ya (W)-    2
Jumla:    4

#.Vikao  vya kawaida  vya Kamati ya Siasa ya Wilaya  vifanyike kila baada ya miezi mitatu badala ya kila  mwezi isipokuwa vinaweza kufanyika vikao maalum inapohitajika.

#. Muundo wa Wilaya za Chama uendane na muundo wa sasa wa Serikali.

Kata,Tawi na Shina
Idadi ya kuanzisha Shina iwe wanachama 50  hadi 300.

Idadi ya kuanzisha Tawi iwe wanachama kuanzia 301 hadi 1,000.
Hata hivyo idadi hii izingatie eneo la kijiografia na wingi wa wanachama katika eneo hilo.

Vikao vya kawaida vya  Kamati za Siasa  za  ngazi hizi viwe vinafanyika mara moja kila baada ya miezi mitatu, isipokuwa vinaweza kufanyika vikao maalum inapohitajika.

#. Nafasi za Uongozi
Mwanachama atakiwe kuwa na nafasi  moja tu ya uongozi wa kazi za muda wote kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni za uchaguzi wa Chama Toleo la 2012 kifungu cha 22 na 23 ambazo zimetajwa kuwa ni:-
Mwenyekiti wa Tawi,Kijiji au Mitaa.
Mwenyekiti wa Kata/Wadi.
Mwenyekiti wa Jimbo, Wilaya na Mkoa.
Makatibu wa Halmashauri Kuu wa ngazi zote zinazohusika.
Mbunge, Mwakilishi na Diwani.

#. Viongozi wa kuchaguliwa waepuke kuwa watendaji badala yake waongoze na kusimamia shughuli za Chama kwa kuzingatia Katiba na Kanuni.

#.Vyeo ambavyo haviko kwenye Katiba
Vyeo  ambavyo havijatamkwa kwenye Katiba ya CCM haviruhusiwi katika Chama au Jumuiya zake mfano Umoja wa makundi mbalimbali kama Wenyeviti wa ngazi mbalimbali (mfano: Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM n.k), Makamanda (UVCCM), Washauri (UWT) na Walezi (WAZAZI) katika ngazi zote.

#. Uhakiki wa Wanachama wa CCM
Ipo haja ya kufanya uhakiki wa wanachama wa CCM  na Jumuiya zake ili kujua idadi sahihi ya wanachama wetu kwa wakati huu.   Uhakiki huu uendane na kutoa kadi mpya za uanachama za kielektroniki ili kuwa na udhibiti wa usahihi wa wanachama na kuondoa wanachama HEWA. Aidha, Kadi za UWT, WAZAZI na UVCCM zifutwe ili tubaki na kadi za CCM tu.

#. Jumuiya za Chama Cha Mapinduzi
Jumuiya za CCM  zimetakiwa kufanya kazi zake kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya CCM na Kanuni za Jumuiya husika, kanuni za Jumuiya ziendane na  matakwa ya Katiba ya CCM.

#.Uaendeshaji  wa shughuli zote za Jumuiya za Chama na mali zake uwe chini ya usimamizi wa Chama Cha Mapinduzi. (Baraza la Wadhamini la Chama Cha Mapinduzi).
Makatibu Wakuu wa Jumuiya wawe wanateuliwa na Kamati Kuu  na  Manaibu Katibu Wakuu wateuliwe na Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa.

#. Wakati tukiendelea kubaki  na Bendera yenye rangi ya kijani na njano  na  alama ya jembe na nyundo ipo haja ya kuzifanya rangi hizo kuwa na muendekano wa kuvutia zaidi.

#. Utumishi  katika  Chama na Jumuiya zake. Katibu Mkuu wa CCM na Sekretarieti ipewe majukumu ya kusimamia ajira za Watumishi wa Chama na Jumuiya zake.

Nafasi za Makatibu Wasaidizi wa Mikoa na Wilaya ziondolewe na badala yake kazi zao zitekelezwe na Makatibu wa Jumuiya  za Chama wa Mikoa na Wilaya kwa utaratibu utakaopangwa.  Utaratibu huu utakipunguzia Chama Cha Mapinduzi gharama na kujenga umoja wa utendaji kazi wa Chama na Jumuiya zake katika Mikoa na Wilaya.

#. Tathimini ya hali ya Kisiasa na  Uchaguzi wa    Zanzibar .
Halmashauri Kuu ya Taifa imeagiza kuundwa kwa Kamati maalum ya kufanya tathimini ya kina kuhusu hali ya kisiasa Zanzibar kwa ujumla na masuala yanayohusu uchaguzi wa Zanzibar 2015.

# Mwenyekiti wa Kamati ya udhibiti na nidhamu ametakiwa akamilishe kazi ya taarifa ya udhibiti kwa wanachama waliokiuka mienendo ya kiuanachama kabla ya kuanza uchaguzi Mkuu wa Chama mwezi Februari 2017, Mikoa na Wilaya ambazo hazijaleta taarifa zao za kiudhibiti ziwe zimefika kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Udhibiti na Nidhamu kabla ya tarehe 30/01/2017.

#. Uhakiki wa Mali za Chama uendelee kufanyika kwa kina na uchambuzi zaidi ukikamilika Taarifa yake iwasilishwe kwa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa mapema iwezekanavyo.

#. Maamuzi haya yatapelekea kufanyika kwa mabadiliko ya Katiba ya Chama na Kanuni za Jumuiya  za Chama.

#. Kwa mambo yale ambayo yatahitaji mabadiliko ya Katiba, Mkutano Mkuu utaandaliwa mapema mwakani na kutafakari na kupitisha mabadiliko hayo ya Katiba.

Aidha Mwenyekiti wa Taifa Dr. John Pombe Joseph Magufuli ameteua wafuatao kujaza nafasi mbalimbali ndani ya sekretarite. Ambazo zimekuwa wazi kutokana na waliokuwa wakizishikilia kupewa majukumu mengine ya kiserikali.

#.Ndg. Rodrick Mpogolo anakuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Ndg. Rajabu Luhwavi ambaye ameteuliwa kuwa balozi.
#. Col. Ngemela Eslom Lubinga- Kuwa Katibu NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Dr. Asha-Rose Migiro aliyeteuliwa kuwa Balozi
#. Hamphrey Polepole kuwa Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Ndg. Nape Nnauye aliyeteuliwa kuwa Waziri.
#. Wajumbe wengine watabaki kama walivyo sasa.

Imetolewa na:-
Nape Moses Nnauye
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
13/12/2016
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top