Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Hizi hapa tetesi za usajili Barani Ulaya

Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya dirisha dogo la usajili wa January halijafunguliwa vilabu kadhaa barani Ulaya tayari vimeanza kuonyesha kuwataka baadhi ya wachezaji flani kutoka vilabu vingine.


● Manchester City wanafikiria kumuuza kipa Joe Hart ambaye yuko kwa mkopo Torino kwa bei ya 'hasara" paundi milioni 10 lakini nje ya timu zinazocheza katika ligi kuu ya England. (Source: Sun Sport)

● Kocha wa Manchester City Pep Guardiola amezungumzia mpango wa kumhamisha Alexis Sánchez kwenda kuichezea timu hiyo (Source: El Mercurio)

● Mesut Özil anataka mkataba mpya Arsenal kwa sharti moja tu la kulipwa mshahara sawa na Pogba yani paundi 290,000 kwa wiki. (Source: Evening Standard)

● Tottenham wamekamilisha mkataba wa matangazo katika jezi zao ambapo sasa watapata paundi milioni 25 kwa mwaka kuanzia msimu ujao toka kwa kampuni ya Nike. (Source: Daily Mail)

● Nyota wa zamani wa Barcelona Eiður Guðjohnsen amesema yuko tayari kuichezea Chapecoense ya Brazil ambayo wachezaji wake walikufa katika ajali ya ndege wiki iliyopita. (Source: @Eidur22Official)

● Julian Draxler ameweka wazi mpango wake wa kujiunga na klabu yoyote katika ligi kuu ya England mwezi January.  (Source: Daily Mail)

● Kocha wa West Brom  Tony Pulis ameweka wazi mpango wa kuwasajili kiungo wa Manchester United Morgan Schneiderlin na mshambuliaji wa Southampton Jay Rodriguez katika dirisha la usajili n January. (Source:Telegraph)

● Tottenham wanafikiria kuwasajili moja kati ya makipa Joe Hart au Jordan Pickford wa Sunderland kama ikitokea kipa wao Hugo Lloris ataihama klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu (Source: Sun Sport)

● Everton, Manchester United na Manchester City zote zimeonyesha nia ya kumsajili beki wa kati wa Southampton Virgil van Dijk. (Source: Sunday Mirror)

● Everton, West Bromwich Albion, Watford na Swansea zote zimeonyesha nia ya kumsajili winga wa Manchester United Ashley Young mwenye miaka 31.(Source: ESPN)

● Liverpool watatakiwa kushindana na PSG ili kupata saini ya kiungo Christian Pulisic mwenye miaka 18 toka Borussia Dortmund.
 (Source: BILD)
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top