Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Majaliwa aonya fedha za Serikali ni za moto

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli inasimamia nidhamu ya kazi na heshima kwa wananchi, hivyo kutaka kila mmoja atimize wajibu wake.

Aidha, imeonya kuwa fedha za miradi ya serikali ni za moto hivyo ziachwe sifanye shughuli zilizokusudiwa, kwani zikichezewa lazima zitaunguza mtu au watu.

Aliyasema hayo jana jioni alipozungumza na wananchi wa Jiji la Arusha waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Alisema serikali imeamua kupanua wigo wa kuhakikisha kila Mtanzania ananufaika na serikali yake kwa kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za serikali.

Alisema serikali inaendelea kuwahudumia wananchi na kuwataka wakurugenzi, wakuu wa mikoa na wilaya kusimamia maendeleo ya wananchi huku akimpongeza Gambo kwa kufanya kazi za kuwahudumia wananchi.

Pia amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo kukutana na watoa huduma wa magari ya Noah yanayosafirisha abiria maeneo mbalimbali ili kutatua changamoto zao ikiwemo usumbufu wa usafirishaji wanaopata.

Alimpongeza kwa kuwezesha kuibua ajira kwa vijana na kumwagiza Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athumani Kihamia kuhakikisha vijana wanapewa maeneo ya kufanya biashara.

Waziri Mkuu pia alitoa rai kwa Halmashauri ya Jiji la Arusha kuangalia jinsi ya kukusanya ushuru kwa kinamama wafanyabiashara wanaotembeza bidhaa zao kwenye mabeseni jijimo humo ili waweze kujikwamua.

Katika mkutano huo, Waziri Mkuu alikabidhi pikipiki zaidi ya 200 kwa waendesha bodaboda ili waweze kujikwamua kiuchumi. Awali, kabla ya Waziri Mkuu kuzungumza na wananchi, Gambo alimpongeza Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro (Chadema) kwa kuungana na falsafa ya Hapa Kazi Tu.

Alisema alipoingia mkoani hapo alikuta Diwani analipwa Sh 150,000 kila mwezi na vocha ya simu Sh 100,000.

“Tuliona hili hapana na tulikata fedha hizo za madiwani tukalipa madeni ya walimu. Kuhusu maeneo ya wazi, tumempa orodha Rais ya hayo maeneo na tunasubiri maamuzi yake kwa ajili ya miradi ya maendeleo,” alisema.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top