Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Nape ajisalimisha .... Awaangukia wapinzani wake

Alikuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amewaomba radhi viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani nchini kwa lolote ambalo aliwakwaza wakati akitekeleza majukumu yake katika nafasi hiyo.

 Image result for NAPE NNAUYE NA MBOWE

Nape Nnauye (Kushoto) akiwa Edward Lowassa wakiteta jambo

Nape amewaangukia wapinzani pamoja na makundi mengine ya watanzania ikiwemo viongozi wenzake ndani ya chama leo wakati akikabidhi rasmi ofisi kwa kiongozi mpya anayechukua nafasi hiyo, ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Dar es Salaam, Humphrey Polepole katika ofisi ndogo za makao makuu ya chama hicho, Lumumba Jijini Dar es Salaam.

"Nawaomba msamaha viongozi wenzangu, wanachama, waandishi na hata wapinzani pale ambapo nimewaumiza katika kufanya kazi yangu, samahani sana. Nategemea ushirikiano niliopatiwa mimi na wanahabari utaendelea kwa ndugu yangu Humphrey Polepole, ni mtu mwenye weledi mpana" amesema Nape

Nape pia amekiri kuwa chama hicho kimemsaidia zaidi kwenye maisha yake kuliko yeye alivyokisaidia wakati akiitumikia nafasi hiyo.

"Nakiri mbele yenu kuwa chama kimenisaidia zaidi kuliko mimi nilivyokisaidia Chama, nashukuru Mungu kuwa nimemaliza kazi hii salama, nilipata wosia wa Mzee Kinana kuwa nishukuru nikimaliza salama"
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top