Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Ronaldo ajitengenezea rekodi yake mpya kwenye soka

Cristiano Ronaldo ameendelea kujitengenezea rekodi yake mpya kwenye mchezo wa soka.

Alhamisi hii mchezaji huyo alifanikiwa kufikisha goli lake la 500 kati ya mechi 638 wakati Real Madrid ikipata ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Club America ya Mexico katika mchezo wake wa nusu fainali ya kombe la vilabu bingwa vya dunia huko nchini Japan.

Magoli hayo yote ni yale aliyofunga akiwa na timu za vilabu pekee, ikiwemo Sporting Lisbon ya Ureno aliifungia magoli matano katika michezo 31, Manchester United alifunga magoli 118 kati ya mechi 292 na timu yake ya sasa ya Real Madrid kashafunga magoli 377katika michezo 366 aliyocheza.

Wakati huo huo Ronaldo ndio mfungaji bora wa muda wote kwenye timu ya taifa ya Ureno akiwa ameshafunga jumla ya magoli 68 mpaka sasa.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top