Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Skendo 10 zilizotikisa 2016

Zimebaki siku chache sana Mwaka wa 2016 uishe. Yapo mengi yametokea mazuri na mabaya, ya kufurahisha na kuhuzunisha, ya aibu na ya heshima!

Katika kuufunga mwaka, tumefanya kitu ambacho unaweza kukiita funga kazi kwani kupitia toleo hili tunakuletea Top Ten za mastaa wa fani mbalimbali waliofanya vizuri kwa mwaka huu.

Pia Top 10 ya viongozi waliong’ara na kuvuma, skendo za mastaa zilizotikisa, misiba iliyoshitua wengi pamoja na nyimbo za muziki wa Bongo Fleva zilizobamba.
Yote hayo utayapata kwenye ukurasa wa 2, 3, 4, 12 na 13.

Abubakar Mzuri
Huyu ni yule mshikaji aliyetokea Shindano la BSS ambaye alitikisa sana mwaka huu kwa skendo ya kufumaniwa akiwa na mke wa mtu akachezea kichapo ile mbaya.

Idris
Jamaa huyu ndani ya mwaka huu amedaiwa kutoka na mabinti wengi kama vile Linah, Sanchoka lakini alikumbwa na skendo ya kutembea na Gigy Money wakati alipokuwa kwenye uhusiano na Wema Sepetu.

Gigy
Aliandikwa sana kwa kupiga picha za nusu utupu, kubadilisha mabwana lakini skendo aliyokanyaga na ikawa gumzo ni ile ya kudaiwa kulala na msanii Tekno kutoka Nigeria pale mwanamuziki huyo alipokuwa nchini kwa shughuli za kisanii.

Shilole
Wakati msanii kutoka Nigeria, Wizkid akiwa jijini Mwanza kwa ajili ya shoo, ilidaiwa kuwa Shilole alijisogeza kwake na kufanikiwa kulala naye kwenye hoteli moja jijni humo.

Amber Lulu
Alitikisa na skendo yake ya kudaiwa kukamatwa na unga jijini Arusha lakini ikazimwa kabla ya juzikati naye kufunga mwaka na skendo ya kurekodiwa video akicheza mtupu kama alivyozaliwa.

Wema
Huyu ni staa ambaye ameandikwa kwa mengi mwaka huu lakini skendo iliyotikisa kwake ni ile ya kudaiwa kutoka kimapenzi na modo aliyefahamika kwa jina la Calissar. Inadaiwa walikuwa ‘wakidate’ kwa siri lakini baadaye ikavuja video ikiwaonesha wakifanya yao chumbani, skendo ikachukua muda mrefu kutrendi kwenye ‘midia’ mbalimbali na kwenye mitandao.

Jike Shupa
Huyu naye hakuwa nyuma kwa skendo. Utakumbuka aliwahi kupigwa picha akiwa hajavaa kufuli na ‘mali zake muhimu’ kuonekana hadharani. Acha hiyo, hivi karibuni pia alijirekodi video akijiridhisha kimahaba, skendo ambao ilionekana kumchafua sana hasa ikichukuliwa kuwa ni mtu mzima mwenye familia.

Barakah The Prince
Anaingia katika orodha hii na skendo yake ya kudanganya kumiliki nyumba. Msanii huyu alijigamba kwenye mitandao na kwenye TV kuwa anamshukuru Mungu na mpenzi wake, Naj kukamilisha nyumba. Hata hivyo, aliibuka msanii mwenye ukaribu na familia ya Naj na kumuumbua kuwa ni nyumba ya mama yake Naj.

Diamond
Huyu naye hajambo kwa skendo lakini kubwa iliyotikisa kwa mwaka huu ni ile ya kumsaliti mzazi mwenzake Zari kwa kudaiwa kutembea na modo aliyefahamika kwa jina la Lynn kisha kumpa mimba. Pia akadaiwa kutembea na Hamisa Mobeto ambaye naye alidaiwa kumpa mimba licha ya baadaye kuja taarifa za kuchoropoka kwa ujauzito huo.

Kidoa
Alianza mwaka na skendo ya kunaswa hotelini na mwanasoka Mbwana Samatta wakifanya yao. Baada ya skendo hiyo kuvuma sana kwa kipindi, katika kufunga mwaka tena akaibuka na nyingine ya kudaiwa kubakwa akiwa kwenye studio moja ya kupiga picha iliyopo Magomeni jijini Dar.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top