Loading...
BREAKING NEWS ... Mgombea Ubunge Chadema atupwa jela miezi nane
Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Lindi Suleiman Mathew Luwongo ambaye pia alikuwa mgombea ubunge wa jimbo la Mtama na Katibu wa CHADEMA tawi la Nyangamara wamehukumiwa kifungo cha miezi nane jela (bila faini).
Kosa walilokuwa wanatuhumiwa nalo ni kufanya mkutano bila kibali. Hukumu imetolewa leo 18.01.2017 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi. Walioshitakiwa walikuwa sita lakini wanne wameachiwa huru.
Ngatunga - Katibu Kanda ya Kusini
Post a Comment