Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

BREAKING NEWS ... Serikali yawabwaga wanaharakati sheria ya mitandao



Na Mwandishi Wetu
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania imetupilia mbali kesi iliyofunguliwa kupinga sheria ya mtandao iliyotungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015 ili kulinda maslahi ya Taifa ya kupambana na kutoa mwelekeo wa kukabiliana na makosa ya mtandao.

Hukumu hiyo ya kihistoria ilitolewa na jopo la majaji watatu, Prof. John Ruhangisa, Winfrida Korosso na Lugano Mwandambo mara baada kuona hoja zilizowalishwa na wakili wa kujitegemea Jebra Kambole kuwa hazina msingi.

Hata hivyo, mahakama hiyo imetoa maelekezo kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kufanya marekebisho kwenye kifungu kimoja kati ya 18 vya sheria hiyo vilivyokuwa vikilalamikiwa kwa vile kifungu hicho kinakiuka haki ya msingi ya mwananchi ya kusikilizwa.

Pamoja na kutoa maelekezo hayo, mahakama imeona vifungu vingine ndani ya sheria hiyo havikuwa na mapungufu yoyote ya kikatiba kama ilivyokuwa inadaiwa na mwombaji (Kambole).

Katika malalamiko yake, Kambole alidai kuwa Sheria ya mtandao ilikuwa na baadhi ya maneno ambayo hayakutafasiriwa ambavyo kwa namna moja au nyingine vingeweza kuchambuliwa vibaya na vyombo vya usalama na hivyo kumwonea mwananchi.

Hata hiyo, jopo la majaji hao waliona hoja hizo hazina mashiko mara baada ya kupitia kwa kina vifungu vya Sheria husika na kuona kuwa vifungu hivyo lalamikiwa vinaainisha kosa ambalo linaweza kutendeka na kutoa adhabu inayotakiwa.

Majaji hao wamebainisha kuwa vifungu namba 4, 5, 6, 7, 8, 9, 14, 19, 21 na 22 vya sheria ya mtandao vilivyolalamikiwa vinaenda sambamba na Ibara ya 17 (2) cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hivyo haviwezi kwenda kinyume na katiba.

Kwa mujibu wa jopo hilo, mwananchi anayonafasi ya kupinga maamuzi yanayotolewa na kiongozi kwa kupeleka maombi ya mapitio (judicial review) mahakama kuu kama itabainika kuwa alienda kinyume na madaraka yake aliyopewa kisheria.

Mara baada ya kufikia uamuzi kuwa vifungu hivyo vya sheria ya mtandao havikinzani na Ibara ya 17 (2), 20 (5) na 30 (2) vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, majaji hao walikataa wito wa mlalamikaji wa kuviona vifungu hivyo vinakiuka katiba.

Kambole katika maombi yake alilalamikia pia vifungu namba 38 na 50 vya sheria ya mtandao kwamba vinakiuka Ibara ya 13 ya Katiba juu ya mwananchi kuwa na haki ya kusikilizwa.

Mlalamikaji huyo alidai kuwa kifungu namba 38 kinatoa uhuru kwa mamlaka kupeleka maombi mahakamani ambayo yanaweza kusikilizwa kupitia upande mmoja bila upande wa pili katika maombi hayo kuhusishwa.


Hata hivyo, majaji hao walibainisha kuwa kifungu hicho kinahusiana na maswala ya kufanya upekuzi, kukamata, kukusanya na kuweka wazi takwimu kwa lengo la upelelezi. Katika mazingira hayo, majaji waliona kuwa malalamiko yaliyotolewa hayakuwa na msingi wowote kwa vile maswala ya upelelezi hayatoi ukomo katika kutatua haki ya mwananchi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top