Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mchungaji mbaroni kwa kumbaka mwanaye

Mchungaji wa kanisa la  Free Pentekoste Church Tanzania (FPCT) Tawi la Gezaulole wilayani Hai, Emanueli Mwikizu (42) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Hai kwa tuhuma za kumbaka mtoto wake  mwenye umri wa miaka 7.

Akisoma hati ya mashtaka mahakamani hapo mbele ya hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Anold Kirekiano mwendesha mashtaka wa polisi, Elisha Moleli amesema mtuhumiwa huyo alitenda kosa la kuzini akijua kufanya hivyo ni kosa la jinai.

Alisema kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo Januari 17 mwaka huu  nyumbani kwake mtaa wa Gezaulo majira ya saa 3:30 asubuhi kwa kumwingilia kwa nguvu na kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri.

Mtuhumiwa huyo alikana shtaka hilo ambapo hakimu anayesikiliza kesi hiyo aliharisha hadi Februari 9 mwaka huu itakapotajwa tena na mtuhumiwa yupo rumande baada ya kushindwa masharti ya dhamana.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top