Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Rais Magufuli: Ni marufuku kumpangia mkulima bei

Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amepiga marufuku viongozi wa serikali wenye tabia ya kuwapangia bei ya mazao wakulima na kuwataka wawaache wakulima wauze mazao yao kwa bei itakayowanufaisha wakulima kutokana na mazao yao

Ameonya juu ya tabia hali ilivyo sasa ambapo mkulima amekuwa akipunjwa kutokana na bei ndogo anayolipwa pindi anapouza mazao yake.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo wakati ambapo amemaliza ziara ya siku mbili mkoani Simiyu na kuanza rasmi ziara ya siku mbili mkoani Shinyanga na kuahidi kuendelea kuulinda Muungano wa Tanzania Bara na  Zanzibar kwa nguvu zake zote

Rais Magufuli amesema Mapinduzi matukufu ya Januari 12,1964 ndio yaliyosababisha kuwepo kwa Muungano kati ya Tanzania Bara na Zanzibar na hivyo kuzaliwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo kuna umuhimu mkubwa kwa  Watanzania kuuenzi na kuulinda kwa manufaa ya wananchi wote.

'' leo ni siku muhimu sana kwetu Watanzania kwa kuwa siku hii ya Januari 12,1964  miaka 53 iliyopita  ndio siku yalipofanyika Mapinduzi matukufu ya Zanzibar yaliyopelekea kuondolewa kwa utawala dhalimu wa kikoloni na kupelekea kuzaliwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya Tanzania Bara na  Zanzibara kuungana,hivyo tuna kila sababu ya kuienzi siku hii muhimu'' amesema Rais Magufuli.

Akiwa Wilayani Maswa mkoani Simiyu mara baada ya kutembelea kiwanda cha kutengenezea chaki na kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa barabara ya Mwigumbi hadi Maswa yenye urefu wa kilomita 50.3 kwa kiwango cha lami, Rais Magufuli amewataka wananchi wa mkoa wa Simiyu kutumia barabara hiyo kujiletea maendeleo.

Rais Magufuli ameupongeza mkoa wa Simiyu kwa kutekeleza kwa vitendo Sera ya Serikali ya awamu ya Tano ya Tanzania ya viwanda kwa ujenzi wa kiwanda cha Chaki na  kutoa wito kwa uongozi wa kiwanda hicho kuongeza uzalishaji wa chaki ili ziweze kukidhi soko la nchi nzima badala ya mikoa kumi ya sasa inayotumia chaki zinazozalishwa na kiwanda hicho.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top