Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Serikali yakanusha uzushi huu ....


Wizara ya Maliasili na Utalii inakanusha taarifa iliyoandikwa na gazeti la Raia Mwema Toleo Na. 494 (ISSN 1821-6250) la Jumatano tarehe 25-31 Januari, 2017 ikiwa na kichwa cha habari “Waziri Maghembe Matatani”. Habari hiyo imeeleza kuwa, Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe anadaiwa kuongeza muda wa leseni za vitalu vya uwindaji kwa kampuni za uwindaji wa kitalii kinyume na taratibu.

Aidha, habari hiyo imeeleza kuwa waziri hakufuata utaratibu uliowekwa katika kifungu cha 38 (6) cha Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 ambayo inaweka utaratibu wa kufuatwa kabla waziri hajatoa leseni upya. Pa, habari hiyo imeeleza kuwa sheria hiyo inataka itangazwe kwenye magazeti utaratibu wa kuomba vitalu kwa waombaji pamoja na kufanyiwa tathmini.

Vilevile, habari hiyo imeeleza kuwa waziri anatakiwa kushauriwa na chombo ambacho ndicho hufanyia tathmini kampuni hizo. Taarifa hiyo imeripoti kuwa hapo awali kulikuwa na kamati ya kumshauri waziri ambayo ilivunjwa mwaka 2012 na aliyekuwa waziri wa Wizara hiyo, Khamis Kagasheki na hivyo kuhoji uhalali wa kufanya maamuzi bila kushauriwa na chombo hicho.

Habari hiyo siyo ya kweli, kwani Waziri hakutoa leseni za umiliki wa vitalu vipya bali ameongeza muda wa umiliki wa vitalu kwa mujibu wa kifungu cha 38 (8) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 sambamba na kanuni ya 16 ya Kanuni za Uwindaji wa Kitalii za mwaka 2015. Sheria na Kanuni hiyo inaelezea utaratibu wa kuongeza muda wa umiliki wa vitalu kwa wale walioomba kuendelea na umiliki wa vitalu vya awali (renewal of hunting block).

Waziri kabla ya kuongeza muda wa umiliki wa vitalu (renewal) alikaribisha maombi kwa wale wanaotaka kuongezewa muda wa umiliki wa vitalu wanavyovimiliki kwa mujibu wa Sheria tajwa hapo juu kwa barua yenye Kumb. Na. CHA.79/519/47 ya terehe 22 Aprili, 2016. Aidha maombi hayo yalipitiwa na Kamati ya Ushauri ya Ugawaji wa Vitalu vya Uwindaji ambayo ipo kisheria na iliteuliwa Septemba 2013, kinyume na madai ya mwandishi kuwa Kamati hiyo haipo. Baada ya tathmini ya maombi hayo, Kamati hiyo ilimshauri Waziri kwa mujibu wa sheria.

Kwa kufuata utaratibu ulioanishwa katika Kifungu cha 38 (8) na (9) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori, kifungu hiki kinampa Mamlaka Waziri kuongeza muda wa umiliki wa vitalu (Renew of hunting blocks). Kanuni ya 16 kanuni ndogo ya (1), (2), (3), (4), (5), (7), (8), (9) na (10) ya Kanuni za Uwindaji wa Kitalii  zinatoa utaratibu wa kufuatwa wakati wa kuongeza muda wa umiliki wa vitalu kwa muhula mwingine wa uwindaji na utaratibu huo umefuatwa.

Kwa kuzingatia utaratibu huo, wamiliki wa sasa wa vitalu kama Kanuni zinavyoelekeza, waliwasilisha maombi yao Wizarani. Idara ya Wanyamapori ilipitia maombi hayo na kuwasilisha kwenye Kamati ya Ushauri ya Ugawaji wa Vitalu vya Uwindaji. Kamati hiyo ilipitia maombi hayo tarehe 26 hadi 27 Julai 2016 na tarehe 13 Januari 2017. Hivyo, baada ya Kamati kukamilisha taratibu zote na kujiridhisha iliwasilisha ushauri wake kwa Mhe. Waziri.

Kifungu cha 38 (6) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori alichokitaja mwandishi wa gazeti hilo, kinaeleza utaratibu wa ugawaji wa vitalu kwa waombaji wapya na siyo kwa wale wanaoomba kuendelea na umiliki wa vitalu kwa msimu mwingine (renewal).
 
Uongezaji wa muda wa umiliki wa vitalu vya uwindaji ulifuata Sheria, Kanuni na Taratibu, Hivyo tunawoamba wananchi wapuuze habari hiyo kwani mwandishi alikusudia kuupotosha umma kwa kunukuu na kutafsiri vifungu vya Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori isivyo sahihi.

Imetolewa na,
KATIBU MKUU
29 Januari, 2017
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top