Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mwanamuziki mkongwe afariki Dunia

Mwanamuziki mkongwe kutoka Msondo Ngoma Music Band, Shaaban Dede amefariki dunia leo saa mbili asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Taarifa hizo zimethibitishwa na mtoto wake wa kiume aliyetambulika kwa jina la Hamad Dede na kusema mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa marehemu Mbagala jijini Dar es salaam, na kwamba ratiba na taratibu zote zitatangazwa mara zitapokamilika kupangwa.

Marehemu Dede atakumbukwa kama mmoja wa wanamuziki nguli kutokea nchini Tanzania kwa uwezo wa kucheza na sauti yake pamoja na kuwa mtunzi mahili wa nyimbo mbalimbali  enzi za uhai wake alipokuwa anaimbia bendi tofauti tofauti ni Jazz, Bima Lee, Tabora Mlimani Park na Msondo Ngoma ambako alikuwa anatumikia hadi mauti yanamkuta.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top