Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Ofisi ya CCM yachomwa moto Pwani

Watu wasiojulikana wameichoma moto ofisi ya Chama cha Mapinduzi tawi la Mshonzini iliyopo wilayani Mafia mkoani Pwani na kuteketeza mali mbalimbali za chama hicho.

Akithibitisha tukio hilo, Katibu wa CCM wilayani Mafia Mohammed Dhikiri amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana  Alhamisi Julai 13.

Dhikiri amesema moto huo umeteketeza kabisa ofisi hiyo pamoja na samani za ndani.

Amesema bado haijajulikana sababu za ofisi hiyo kuchomwa moto kwa kuwa wakati tukio linatokea hakukuwepo na viashiria vyovyote vya vurugu miongoni mwa wanachama.

Amesema bado halijafahamika ni nani aliyehusika na tukio hilo na kueleza kuwa wameliachia Jeshi la Polisi kuendelea na uchunguzi zaidi dhidi ya tukio hilo.

Naye  Mbunge wa Mafia, Mbaraka Dau amesema vipo viashiria vinavyoonyesha kuwa alifika mtu asiyejulikana karibu na ofisi hiyo kisha kuwasha na kurusha kijinga cha moto kwenye paa la makuti la ofisi hiyo.

Dau amesema mtu huyo baada ya kutekeleza kitendo hicho aliondoka kuelekea kichakani kama ambavyo alama za nyayo za miguu yake zilivyoonyesha.

Amesema hilo ni tukio la kwanza kutokea wilayani humo kwa kuwa hadi linatokea hapakuwa na viashiria vyovyote vile vya kutokuwepo kwa Amani kati ya wanachama au viongozi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top