Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Wabunge wa Chadema wataka kumpiga Mbunge wa CCM .... Wakamatwa

Mbunge Juliana Shonza


Habari  kutoka  mjini Dodoma  zinaeleza  kuwa  wabunge kadhaa  wa  chama  cha  Demokrasia na maendeleo  (CHADEMA) ambao  walikwazika  na  uchangiaji  wa mbunge  wa  CCM Juliana  Shonza  na  kutaka kumpiga  wakati  mbunge  wa Kawe  Halima  Mdee  alipokuwa  akipewa adhabu  kwa  kutoa  lugha  chafu  bungeni wamekamatwa .


Taarifa zilizoufikia  zinadai kuwa wabunge  hao   walikamatwa jana  majira  ya  usiku baaada ya  bunge kuarishwa  na baada ya  kukamatwa  walifikishwa  polisi  na bado  haijajulikana  iwapo  waliachiwa ama  lah.

Idadi  ya  wabunge  waliokamatwa  inasadikika  kufikia zaidi ya  watano ,mtandao   huu  unaendelea  kumtafuta  kamanda  wa  polisi mkoa wa Dodoma  ili  kuthibitisha  kukamatwa  kwa  wabunge  hao.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top