Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KISA CHA MWANAMUZIKI DAIMOND PLATNUM NA SIASA ZA WAPINZANI NCHINI


Image result for diamond platnumzKISA CHA MWANAMUZIKI DAIMOND PLATNUM NA SIASA ZA WAPINZANI NCHINI

Mwanamuzi wa kizazi kipya nchini Abdul Nassib almaarufu kama Daimond Platnumz amekuwa kwenye vichwa vya habari siku za hivi karibuni kufuatia kutuhumiwa kuzaa na Mwanamitindo Hamisa Mobeto ambapo yeye Hamisa alikiri kuzaa nae lakini Daimond Platinum alikuwa akikataa kataa mpaka leo hii Jumanne Septemba 19, 2017 Daimond Platinum akiri kwa mara ya kwanza kuzaa na Hamisa Mobeto.
Daimond Platnum ameanika uhusiano wake na Hamisa wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Leo tena cha Cloudsfm. Daimond Platnumz akiri Mtoto ni wake na alianza kuihudumia mimba toka siku ya kwanza. Kila siku Hamisa Mobeto alikuwa anaenda kushinda Madale; Diamond Platinumz amekiri kumnunulia gari aina ya Rav 4 Hamisa wakati akiwa mjamzito kwa ajili ya kumpeleka kliniki; Diamomd humpa Hamisa Tsh. Laki 5 kila wiki ya matumizi; Diamond Platinumz alimpa Tsh. Milioni 7 Hamisa kwa ajili ya kununua vitu vya Mtoto na samani za ndani; Siku Diamond Platnum anarudi kutoka London alienda kulala na Mwanaye na kushinda nae.
Daimond Platnum amekuja kukiri dakika ya mwisho mara baada ya kuona Hamisa anaanza kuvujisha picha zao wakiwa faragha na kuona itamchafulia.
Kisa hiki cha Daimond Platnumz nakifananisha na kisa cha Wanasiasa wetu hapa nchini hususani wale wa vyama vya upinzani wasiopenda kuongea ukweli wa mambo kwa wakati na kungojea tukio lipite ndio kuja kukiri ukweli. Hii tabia ya kubadilika badilika haina tofauti na tabia au hali ya unafki.
Tuweke kumbukumbu zetu sawa. Mwalimu Julius Nyerere wakati akiwa madarakani alimwagiwa lawama na tuhuma lukuki kwani wapo waliosema Mwalimu haambiliki na wengine wakadai anaendesha nchi kwa “remote” akiwa Butiama (kijijini kwao). Lakini mara baada ya kung’atuka kwa hiari Urais ndipo sifa za kinafki zilianza kummiminikia huku tukianza kumuita “Baba wa Taifa”. Mara baada umauti kumkuta ndipo unafki ulizidi kwake na leo hii kila kitu kibaya kinachotokea tunasema laiti Mwalimu Nyerere angekuwepo haya yote yasingetokea. Lakini angali hai ama madarakani hatukuyatambua haya zaidi ya kuuendekekeza unafki.
Ama Alhaji Hassan Mwinyi wakati akiwa Rais wa awamu ya pili walimwita mbinafsi, muuzaji nchi kutokana na ubinafsishaji lakini leo hii ni mstaafu wanaanza kummwagia sifa teletele  na hata kumwita “Mzee wetu” huku wakijivunia kuchota hekima na busara kutoka kwake lakini angali madarakani hatukuliona hilo. Huu ni unafki mtupu.
Pia Mzee  Benjamini Mkapa alidhihakiwa kweli kweli wakati wa uongozi wake hadi kufikia hatua ya kumwita ‘ukapa’ badala ya Mkapa kutoka katika neno la ‘ukata’. Lakini leo hii kila anapokatiza ni shangwe, makofi, vifijo, na vigelegele na tukisema afadhali ya Mkapa kuliko wote na wengineo tumewaona wakimpa hata tuzo ya heshima. Jamani! Kama huu si unafki, basi tuuiteje?
Hata Dk. Jakaya Kikwete (JK) alipokuwa madarakani walimuita majina mengi ya hovyo hovyo. Wapo waliomuita “Mzee wa kutabasamu”, Serikali yake ni dhaifa na legelege! Lakini hekima na busara kubwa aliyojaaliwa Dk. Kikwete hakuweza kuwajibu lolote waliokuwa wakimkejeli na badala yake aliwaambia mtanikumbuka.
Kikwete alisema: “Mtaumbuka baada ya 2015”. Dk. Kikwete aliwaambia wanaombeza sasa wataona aibu baada ya kumaliza kipindi chake. Naam! Ni kweli Watu waliokuwa wakimbeza wameanza kuumbuka na kunza kupayuka hadharani kuwa wana mkumbuka.
Kama kweli maisha yalikuwa mazuri kwanini walikuwa wakimkashifu mtu (JK) ambaye amewanyooshea Watanzania maisha yao? Kulikuwa kuna sababu gani kwa Wapinzani kumfedhehesha majukwaani kwamba Serikali yake ilikuwa dhaifu na maisha yalikuwa magumu? Leo hii wanamponda Rais Magufuli, kwanini tusiamini kwamba akitoka madarakani nae wataanza kumsifia?
Rais Magufuli anafanya mambo mengi ya msingi kwa Taifa letu lakini Watu kwa maslahi yao binafsi wanaamua kupindisha ukweli wa mambo tofauti na uhalisia waujuavyo moyoni mwao. Hakuna asiyejua namna ambavyo Rais Magufuli anavyojitahidi kutekeleza ilani ya uchaguzi.
Tangu Rais Magufuli aingie madarakani tumeshuhudia Elimu Bure ikitolewa kuanzia ngazi ya shule ya msingi mpaka Sekondari, Mikopo ya elimu ya juu ikiongezwa na kutolewa kwa wingi, Wanafunzi wa vyuo vikuu wakijengewa hostel za kuishi, madawati yakisambazwa mashuleni, maabara na maktaba zikijengwa mashuleni.
Ni katika utawala wa awamu ya 5 ya Serikali ya Rais Magufuli tumeshuhudia vitanda, madawa na vifaa tiba vikipatikana kwa wingi mahospitalini, huduma bure ya matibabu kwa Wazee na utolewaji wa Bima za Afya ukifanyika, Hospitali zetu hapa nchini zikitoa huduma za kibingwa za upasuaji wa figo, moyo na magonjwa mengineyo hapa nchini, Serikali ikiboresha huduma za Mama Mjamzito na Watoto hapa nchini, Serikali ikiboresha miundombinu ya hospitali na vituo vya afya nchini kwa kuhakikisha huduma za kiafya zinapatikana jirani na wanapoishi na ziwe za uhakika.
Rais Magufuli amehakikisha Taifa letu linakuwa kiuchumi na hatimaye kufikia uchumi wa kati kwa kufufua mashirika ya umma yaliyokuwa yamesinzia kwa mfano kununua ndege mpya 4, kununua hisa zote za kampuni ya simu nchini ya TTCL na hivyo kumilikiwa na Serikali kwa asilimia 100 hali iliyopelekea kampuni kuanza kufufuka; kufufua kilimo kwa kuondoa kodi kwenye kilimo; Kuhakikisha anapambana na madaw ya kulevya nchini; Kuhakikisha rasilimali zetu zinamnufaisha Mtanzania, mfano kwenye sekta ya madini; Kujenga miundombinu ya Barabara, vivuko, madaraja, boti, viwanja vya ndege, ujenzi wa reli ya kisasa ya hadhi ya standard gauge, kujenga barabara za juu (flyovers); Kutengeneza fursa nyingi za ajira kwa kuwatoa wasio na ajira halali na kuajiri wanaostahili kulingana na sifa zao.
Rais Magufuli ameendelea kuhakikisha anapunguza anasa Serikali kwa kuongeza pesa zaidi za kwenye miradi ya kimaendeleo; Kupunguza kiwango cha rushwa nchini; Kuboresha kiwango cha utendaji na uwajibikaji kwa Watumishi wa umma; Kuwaondoa kazini mara moja wale wote wanaoleta mzaha kazini.Hayo ni kwa uchache sana wa mema yanayofanywa na Serikali ya Rais Magufuli.
Kiukweli Serikali ya awamu ya 5 ya Rais Magufuli inachapa kazi sana lakini ajabu yake mara kwa mara asilimia kubwa ya Wapinzani wameshindwa kukubali utendaji wa Serikali ya Rais Magufuli unaofanywa kwa sasa lakini akishatoka madarakani utaona watakavyomsifia, Matukio ya kihistoria yanaonyesha hivyo.
Nampongeza Mwanamuziki Daimond Platnum kwa kuonyesha ukomavu na ushujaa wa kukiri hadharani juu ya Mtoto kuwa amezaa na Hamisa Mobeto kuwa ni wake na hakuwa na sababu ya ziada kuendelea kusema uongo ili kupindisha ukweli. Ni wakati hata kwa vyama vya upinzani, Wanaharakati nao pia kuiga mfano wa Mwanamuziki Daimond Platnumz kukubali kusema ukweli mapema na kwa wakati, kuwa Mpinzani haina maana kupinga kila kitu. Uzalendo huanza kwa kusema ukweli, tuwe wazalendo.
Na Emmanuel J. Shilatu
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top