Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Waziri wa Ujenzi atoa agizo hili

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa ameliagiza baraza la ujenzi nchini kuhakikisha linaandaa taarifa kamili kuhusuiana na ujenzi ili kuondoa changamoto mbalimbali zinazojitokeza mara kwa mara pindi miradi inapotaka kuanza.

Prof. Mbarawa amesema hayo leo katika kikao chake na baraza la ujenzi, ambapo kimewakutanisha wataalamu wa ujenzi kutoka ndani na nje ya nchi kwa lengo la kuangalia changamoto zilizopo kwenye sekta hiyo na kuzitafutia ufumbuzi.

"Kwa sasa hakuna taarifa sahihi kuhusu masuala ya ujenzi nchini, sekta ambayo inachangia kwa asilimia 14 ya pato la taifa na haikui kiushindani na nchi zilizoendelea kwa kiwango cha kisasa", amesema Prof. Mbarawa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Ujenzi nchini, Prof. Mayunga Mkunya amesema hakuna ushirikiano mzuri katika sekta ya ujenzi hali ambayo inachangia kukosa kuwa na mipango endelevu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top