Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mdogo wa Steven Kanumba Atoa Ushahidi Mahakamani Jinsi Kanumba Alivyofariki

Kesi ya mauaji inayomkabili muigizaji wa filamu bongo Elizabeth Michael (Lulu) imeendelea kusikilizwa  jana katika Mahakama Kuu jijini Dar es salaam, kwa upande wa mshataka kuanza kutoa ushahidi wao.

Akitoa ushahidi ndugu wa marehemu Steven Kanumba, Seth Bosco, alisimulia mahakama jinsi ilivyokuwa siku ya tukio, na kwamba aligundua kuwa kaka yake hapumui baada ya kugombana na mpenzi wake Lulu.

"Siku ya tukio marehemu Kanumba alinambia nisitoke nyumbani anataka tutoke wote kuanzia saa sita usiku, akaja Lulu na Kanumba ndiye aliyemfungulia mlango Lulu, alipofika ndani nikasikia akimuuliza Lulu kwanini anaongea na boyfriend wake mbele yake? Katika malumbano yao Kanumba alikuwa akimvuta Lulu arudi ndani na Lulu naye alikuwa anataka kutoka nje, wakati wakiendelea kugombana mlango wa chumba changu sikuufunga”, alisikika Seth akiisimulia Mahakama.

Seth aliendelea kusimulia kuwa …..”Baada ya ugomvi Lulu alikuja chumbani kwangu akilia, akanambia Kanumba kadondoka amejaribu kummwagia maji haamki. Na ilikuwa mara ya kwanza kuona ugomvi kati yao, nilipoingia chumbani nilimkuta Kanumba chini kaegemea ukuta nikamlaza chali nikamtafuta daktari wake, Dk Kageiya, alipofika alimfanyia chek up akanambia ameshafariki ila akashauri tumpeleke hospitali ya Muhimbili”..

Hata hivyo, alipoulizwa na moja wa wazee wa Baraza, Rajabu Mlawa baada ya kutoa ushahidi wake, kama anajua aliyesabisha kifo cha msanii huyo, shahidi huyo alisema hajui.

Mzee wa Baraza: Katika kumchunguza kwako marehemu baada ya tukio hilo, ulibaini kwamba marehemu alipata madhara gani?

Shahidi: Madhara niliyoyabaini ni kukosa pumzi

Mzee wa Baraza: Hayo madhara ya kukosa pumzi yalisababishwa na ugomvi ule?

Shahidi: Kwa hilo mimi siwezi kujua nini kilisabisha kukosa pumzi.

Mzee wa Baraza: Umesema kuwa ulipokwenda chumbani kwa marehemu ulimkuta ameanguka akiwa ameegemea ukutani, unajua ni nani alisababisha tukio la kuanguka?

Shahidi: Siwezi kujua ni nani aliyesababisha kwa sababu mimi sikuwemo mle ndani

Wakati akihojiwa na wakili wa mshtakiwa, Peter Kibatala, kama alikuwepo wakati sampuli za mwili wa marehemu zikichukuliwa kwa ajili ya vipimo vya maabara, kama ilivyoandikwa kwenye maelezo yake, alisema hakuwepo.

“Mimi sikuwepo wakati wa kuchukua sampuli za mwili wa marehemu. Alikuwapo ndugu yangu mwingine, mimi nilikuwepo kwenye mostmortem (taarifa ya kitabibu ya chanzo cha kifo) ya kawaida.”

Wakili Kibatala: Kwa hiyo aliyeandika hapa alikuwa akibuni?

Shahidi: Siwezi kusema kuwa alikuwa akibuni, labda kama ungemuuliza mwenyewe.

Wakili: Katika maelezo yako Polisi ambayo uliyaandika muda mfupi tu wakati wa tukio, kuna mahali ulipoeleza polisi kwamba ulipokwenda kumfuata Dk Paplas ulimwambia mshtakiwa abaki na marehemu?

Shahidi: Hakuna mahali ambapo kuna kipengele nilipomweleza polisi kuwa nilimuacha Elizabeth Michael na marehemu (Baada ya kusoma maelezo yake)

Hata hivyo, alipoulizwa tena na Wakili wa Serikali, George kuhusu kuwepo kwa tofauti ndogondogo katika maelezo yake aliyoyaandika polisi na yale aliyoyatoa kwenye ushahidi wake mahakamani, shahidi huyo alieleza kuwa yeye alikuwa akihojiwa tu na aliyekuwa akiandika ni askari.

Kesi hiyo inayosikilizwa na Jaji Sam Rumanyika iliahirishwa na itaendelea tena leo kwa mashahidi wengine wa upande wa mashtaka kutoa ushahidi wao.

Awali Wakili George aliieleza mahakama kuwa alitegemea kuwa na mashahidi wawili jana, akiwemo Dk Kageiya, lakini wakati wakifanya mazungumzo na shahidi huyo, aliwaeleza kuwa hajisikii vizuri na kuomba atoe ushahidi wake kesho.

Pia Wakili George aliileza mahakama kuwa wataomba kuongeza shahidi mwingine ili wafikie watano.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top