Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

David Kafulila ala kiapo rasmi cha kujiunga na CCM

David Kafulila akila kiapo cha kujiunga na CCM mbele ya Katibu Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole
.….

Baada ya kutangaza kujivua uanachama wa CHADEMA siku Jumatano, David Kafulila leo amekabidhiwa kadi ya CCM.

Kafulila amekabidhiwa kadi ya CCM na Katibu Mwenezi wa CCM, ndg Humphrey Polepole katika mkutano wa kumnadi mgombea wa udiwani wa chama hicho, Kata ya Mbweni jijini Dar es salaam.

Hapo awali Kafulila aliwahi kuwa mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendelo kisha kufuzwa baadae akajiunga na Chama cha NCCR Mageuzi ambapo alifanikiwa kuwa Mbunge wa Kigoma Kusini mwaka 2010-2015 na baadaye kurudi tena Chadema 2016 na hapo juzi jumatano alitangaza kukihama chama hicho kwa madai upinzani hauna nia ya kupambana na ufisadi.

Kwa upande wa mkewe ambaye ni Mbunge Viti Maalumu kupitia chama cha CHADEMA,Jesca Kishoa jana wakati akizungumza na wanahabari alipingana na kauli ya mumewe na kusema kwamba, mumewe anapaswa kusema ukweli na kwamba sababu alizozisema sizo zilizomuondoa ndani ya chama hicho huku akiongeza kwamba mume wake hana msimamo.

Kafulila amekabidhiwa kadi hiyo ya CCM iliwa imebaki siku moja kabla ya kuhitimishwa kwa kampeni za uchaguzi wa marudio ya nafasi za udiwani kwa Kata 43 ndani ya Tanzania
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top