Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Kilichosemwa kwenye ufunguzi wa kikao cha NEC CCM



YALIYOSEMWA LEO JUMANNE NOVEMBA 21, 2017 KWENYE KIKAO CHA HALMASHAURI KUU YA CCM (NEC) TAIFA, IKULU

1. “Waliojitokeza kugombea nafasi mbalimbali ni 3004 na nafasi za wanaohitajika ni nafasi 201” – JPM

2. “Tulifanya magaeuzi makubwa ili kukirejesha chama kwa Wanachama na kurejesha imani ya CCM kwa Watu” – JPM

3. “Mageuzi haya yamekuwa miiba mikali kwa waliozoea kukichezea chama chetu” – JPM

4. “Kila siku Watu wanarejea CCM, ni ishara ya kupendwa vilivyo kwa CCM” – JPM

5. “CCM inahitaji viongozi wanaochukizwa na rushwa, uonevu, ubadhilifu. Wanaopenda kutimiza ahadi za TANU” – JPM

6. “Wajumbe msije na majina yenu mifukoni, mnaweza kurudi nayo yakiwa huko huko mifukoni” – JPM

7.  “Nina imani na uchambuzi uliofanywa na Sekretariet. Kwa wale ambao hawataridhishwa na mgombea yeyote, nimekuja na mafaili ya wagombea wote nitamwonyesha” – JPM

8. “Hapa ni kwenu, bila ya nyinyi (Wajumbe) nisingefika hapa.  Mna kila sababu ya kufanya kikao hapa" - JPM

9. “Katika siku za hivi karibuni tumeona mapinduzi ya kiutawala, kiitikadi, kiuchumi” – Dk. Mkumbo

10. “CCM ndio chama pekee kinachoonekana kina nguvu hapa nchini” – Dk. Mkumbo

11. “Nimekubali kurudi kwa dhati, ninaomba ridhaa nirudi mnipokee” – Lawrence Masha

12. “Nimerudi zizini nikiwa na mkia, nipo tayari kutumika” – Lawrence Masha

13. “Yale tuyotarajia Wapinzani tuyaone yakifanyika, yanafanyika katika utawala wako Rais Magufuli, tuna kila sababu ya kukuunga mkono” – Samson Mwigamba

14. “Kadri wanavyopiga kelele, ndivyo wewe unazidi kupanda mlima” – Samson Mwigamba

15. “CCM ni chama kinachoonyesha kuwajali watu, mimi kama kijana ninajivunia kuwa Mwanachama wa CCM” – Alberto Msando

 16. “CCM kilihaidi kupambana na umaskini, kutengeneza ajira, kurudisha nidhamu na uwajibikaji. Tuna kila sababu ya kupongeza kwa haya mambo mazuri” – Alberto Msando

17. “Leo hii nasaliti ubinafsi, ukabila, umimi kwa kuamua kujiunga na CCM” – Patrobasi Katambi

18. “Upinzani wa leo unajadili mambo binafsi na matukio kuliko kujadili namna ya kulisaidia Taifa” – Patrobas Katambi

19. “Kijana ndani ya upinzani ni karai linalojenga ghorofa. Karai huonekana takataka baada ya ghorofa kukamilika” – Patrobasi Katambi

IMEANDALIWA NA;

Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi
UVCCM TAIFA
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top