Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Rais Magufuli Kamteua Abdulrahman Kinana Aendelee Kuwa Katibu Mkuu CCM

Katibu mkuu wa Chama  Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana leo ameteuliwa na Mwenyekiti wa Chama hicho, Rais John Pombe Magufuli  kuendelea kuwa katika nafasi yake kwa kipindi kingine.

Akiongea katika mkutano wa 9 wa Chama hicho unaoendelea mkoani Dodoma amemshukuru kwa kazi yake nzuri  kwa muda wote ambao amekuwa  katika nafasi hiyo huku akiweka wazi kuwa ni lazima aendelee kufanya nay kazi kwasababu ameridhishwa na utendaji wake wa kazi.

''Namshukuru ndugu Kinana kwa msaada wake mkubwa alionipa kwa kipindi chote hicho nafikiri  anafaa kuendelea kuwa katika nafasi hiyo kwa kipindi kingine,'' amesema Magufuli. 

Kauli ya Rais Magufuli inaondoa tetesi zote zilizokuwa zinadai kuwa Kinana ameandika barua ya kuomba kujiudhuru katika nafasi yake kwa kilichodaiwa kuwa haridhishwi na utendaji wa Mwenyekiti wake Rais Magufuli.

Baada ya kupata nafasi  hiyo Abdulrahman Kinana amemshukuru Rais Magufuli kwa kumuamini pamoja na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kukijenga chama hicho pamoja na nchi  kwa ujumla.

Kinana aliwahi kuwa mtumishi wa Jeshi la Tanzania kwa miaka 20 pamoja na kuwa Spika wa kwanza wa Bunge la Afrika Mashariki mwaka 2001 hadi 2006, amechaguliwa kuwa Katibu mkuu wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM), tangu 2012.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top