Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Wafuasi 28 wa CHADEMA Waliokamatwa Wakiandamana Kinondoni Wafikishwa Mahakamani

Watu 28 wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Chadema wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakituhumiwa kufanya mkusanyiko usio halali na kinyume na sheria.

Washtakiwa hao wamefikishwa mahakamani hapo mbele ya hakimu mkazi, Godfrey Mwambapa na kusomewa shtaka la kufanya mkusanyiko usiyo halali na Wakili wa serikali, Faraji Nguka

Wakili Faraji Nguka, amedai kosa hilo wamelitenda February 16, 2018 barabara ya Kawawa maeneo ya Kinondoni Mkwajuni ambapo walifanya mkusanyiko usio halali wakiwa na nia ya kusababisha uvunjifu wa amani.

Baada ya kusomewa kosa hilo washtakiwa walikana ambapo Wakili Nguka ameeleza kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Hata hivyo, Hakimu Mwambapa alitoa masharti ya dhamana kwa washtakiwa ambapo wametakiwa kuwa na mdhamini mmoja atakayesaini Bondi ya Sh.Milioni 1.5

Washitakiwa hao wamerudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 3, 2018 itakapotajwa.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top