Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

DONDOO ZA SENSA - 3

 Sensa ya watu na makazi ni utaratibu wa kukusanya, kutambua na kusambaza takwimu za kidemokrafia, kiuchumi na kijamii kuhusiana na watu wote na makazi yao nchini katika kipindi maalum.

Watu gani wanaostahili kuhesabiwa wakati wa    sensa ?

            Wakati karani wa sensa atakapopita kwenye kaya ( eneo amabalo watu kwa kawaida huishi na kula pamoja) atawahesabu watu wote waliolala katika kaya husika usiku wa kuamkia siku ya sensa ni lazima wahesabiwe. Usiku wa kuamkia siku ya sensa ni usiku wa siku ya Jumamosi, tarehe 25 Agosti 2012, kuamkia siku ya Jumapili tarehe 26 Agosti, 2012. Hii ina maana kwamba wale wote waliolala katika kaya hiyo usiku wa kuamkia Jumapili ya tarehe 26Agosti, 2012 wahesabiwe kwenye kaya hiyo.

            Kundi lingine litakalohesabiwa ni wale wote ambao hawakulala katika kaya hiyo usiku huo wa kuamkia siku ya sensa lakini walikuwa wamekwenda shamba kulima, kuvuna, kuwinda, machungani au wako katika kazi za usiku na waliolala kwenye msiba wa jirani na kaya zao. Kundi hili ni la wale ambao huwa wanarudi nyumbani asubuhi baada ya kazi za usiku.

            Walio katika kaya za jumuiya ( kaya za pamoja kama vile hoteli, magereza, mabweni, hospitali) ambao walilala kwenye kaya hizo usiku wa kuamkia siku ya sensa.

            Wageni, watumishi na watu wote wasio na makazi maalum au wale wanaohamahama, ambao walilala nchini usiku wa kuamkia siku ya sensa.

            Watu wote ambao siyo raia lakini wanaishi nchini na walilala nchini usiku wa kuamkia siku ya sensa. Kundi hili pia litawahusha mabalozi wa nchi za nje watakaolala nchini usiku wa kuamkia siku ya sensa, nao pia watahesabiwa.

            Wasafiri ambao wako kwenye meli, magari, ndege ,,,,ambao walikuwa nchini usiku wa kuamkia siku ya sensa bila kujali kama vyombo hivyo ni vya hapa nchini ama ni vya nje ya nchi.

            Pia watoto wote waliozaliwa kabla ya saa 6 usiku wa kuamkia siku ya sensa na watu wote waliokufa baada ya saa 6 usiku wa kuamkia siku ya sensa wanastahili kuhesabiwa na wana vipengele ama sehemu zao za kujaziwa.

Watu gani hawastahili kuhesabiwa wakati wa sensa?

            Sio kila mtu ana haki ya kuhesabiwa wakati wa zoezi la sensa, kwani wapo ambao zoezi hili haliwahusu kutokana na kuonekana watachangia kupoteza lengo zima la sensa ambalo ni kupata takwimu sahihi za idadi ya watu na makazi.

            Watu ambao hawastahili kuhesabiwa ni watoto waliozaliwa baada ya saa 6 usiku wa kuamkia siku ya sensa na wale wote walikufa kabla ya saa 6 usiku wa kuamkia siku ya sensa.

            Pia watu ambao wanaishi nje ya nchi lakini kazi na shughuli za kikazi kuvuka mipaka na kuingia nchini kufanya kazi kila siku na kila jioni hurudi nchini kwao hawatastahili kuhesabia.

            Halikadhalika kuna Watanzania wote ambao wako nchi za nje na ambao hawakulala nchini usiku wa kuamkia siku ya sensa .
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright 2025 EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG | Designed By Code Nirvana