Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Rais Kikwete amteua Winfrida Korosso Kuwa Katibu Wa Tume Ya Kurekebisha Sheria Nchini.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bibi Winfrida Beatrice Korosso kuwa Katibu wa Tume ya Kurekebisha Sheria nchini.

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatano, Agosti 22, 2012 mjini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) Balozi Ombeni Y. Sefue kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inasema kuwa uteuzi huo ulianza Agosti 14, mwaka huu, 2012.

Kabla ya uteuzi wake, Bibi Korosso alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Mkurugenzi wa Mashtaka katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam.

Imetolewa na: Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.  Dar es Salaam.
22 Agosti, 2012
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright 2025 EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG | Designed By Code Nirvana