Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MUASISI WA CHAMA CHA NCCR MAGEUZI AFARIKI DUNIA ARUSHA


Naibu Katibu Mkuu kwa upande wa Zanzibar, Mussa Kombo Mussa
……………………………………………..
ALIYEKUWA muasisi wa Chama cha Mageuzi ya Kitaifa (NCCR-Mageuzi), Emmanuel Petro Ole Sirikwa amefariki dunia juzi kwenye hospitali ya AICC jijini Arusha  alikokuwa amelazwa akisumbuliwa na maradhi ya kiharusi.
 
Akizungumza na wandishi wa habari kwenye ofisi za Chama hicho jijini Dar es Salaam jana Naibu Katibu Mkuu kwa upande wa Zanzibar, Mussa Kombo Mussa, alisema chama kimepoteza mwanamageuzi wa kweli katika ulingo wa siasa nchini.
“Chama kimempoteza mtu muhimu, alikuwa ndiye kinara alikuwa miongoni mwa wanchama mwenye kadi  Na. 3 za mwanzo kwani waliokuwa na kadi Na.1 na Na. 2,  ni wale waliyojiingiza kwenye misuko suko ya kijamii, kisiasa na kiuchumi  iliwafanya wamsaliti mtoto waliyemzaa (NCCR-Mageuzi) na kukimbilia vyama vingine”alisema Mussa.
 
Mussa alisema  Ole Sirikwa alifariki usiku wa kuamkia Oktoba 28 mwaka huu katika hospitali  hiyo, ambako  alilazwa kwa majuma mawili baada ya kuugua ugonjwa huo kwa muda mfupi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top