Mkurugenzi wa Idara ya Habari( MAELEZO)Assah Mwambene kushoto akifungua Warsha kuhusu umuhimu wa Lugha ya Alama katika Utoaji huduma kwa Viziwi kwenye Ukumbi wa World Family of Radio Maria,Regency Estate mjini Dar es Salaam na kulia ni Mkalimani wa Lugha ya Alama.
(PICHA NA ANNA ITENDA WA MAELEZO)
Mkuu wa wa Idara ya Wanawake Chama Cha Viziwi Tanzania( CHAVITA)Lupi Maswanya Mwaisaka akitoa neno la Shukrani kwa Mgeni Rasmi Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Ndugu Assah Mwambene wakati wa kufungua Warsha kuhusu Umuhimu wa Lugha ya Alama katika utoaji huduma kwa Viziwi kwenye Ukumbi wa World Family of Radio Maria uliopo Regency Estate mjini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya Washiriki kutoka Vyama na Asasi za Viziwi nchini ,Serikalini na kutoka Mashirika mengine ya kiraia wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO )Ndugu Assah Mwambene (hayupo pichani )akifungua Warsha kuhusu umuhimu wa Lugha ya Alama katika Utoaji huduma kwa Viziwi kwenye Ukumbi wa World Family of Radio Maria mjini Dar es Salaam .
Baadhi ya washiriki wa Warsha kuhusu Umuhimu wa Lugha ya Alama katika utoaji huduma kwa Viziwi kwenye picha ya pamoja na mgeni Rasmi Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Ndugu Assah Mwambene wa sita kushoto (aliyevaa suti) kwenye Ukumbi wa World Family of Radio Maria ,uliopo Regency Estate mjini Dar es Salaam
on Friday, September 28, 2012
Post a Comment