Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

BAVICHA YAPEEWA SOMO


Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Mwanza Liberatus Mulebele Bonventura akimkaribisha Mgeni rasmi kwa ajili ya kufungua semina kwa viongozi wa Bavicha wa Mkoa wa Mwanza katika ukumbi wa iliyokuwa Kivulini Isamilo Mwanza.
………………………………………….
Viongozi wa Baraza la Vijana Chadema Bavicha wametakiwa kuwa tayari kusimamia miiko na sera za chama cha Demokrasia na Maendeleo  ili waweze kuwasaidia Wananchi wa Tanzania ambao wamekosa matumaini kutokana na sera mbaya za Chama cha Mapinduzi ambazo zimeshindwa kuleta msaada kwa Wananchi kwa miaka hamisini toka Tanzania ipate uhuru.
Hayo yamesemwa na Mratibu wa Bavicha Taifa Mheshimiwa Rafiki Lufunga ambaye alikuwa  Mgeni rasmi  katika kufungua mafunzo kwa wa Viongozi wa Bavicha Mkoa wa ili kuwapa uwezo na uelewe jinsi gani waweze kuwasidia Watanzani wote ambao wana mahitaji mengi ambayo hayajatekelezwa ili kuwafanya waishi maisha mazuri.
Amesema Viongozi wa Chadema Wamefanya mambo mengi mazuri na wengine wao wanazidi kuwa wazee hivyo Vijana wasioandaliwa vizuri watashindwa kuleta msaada kwa Watanzania ambao wako njia panda kutokana na utawala ulioko madarakani kushindwa kabisa.
Mwezeshaji wa Semina hiyo Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la Chadema Mzee Silvesta Masinde amesema semina hii imeshafanyika katika Mikoa mbalimbali ya Tanzania na sasa ni zamu ya Mkoa wa Mwanza na Wilaya zake zote, na kuongea kuwa wanachofanya Chadema ni kuwaimarisha Vijana maana wanaamini nguvu ya Chadema iko kwa Wananchi ambao wengi ni Vijana.
 Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Mwanza Revocatus Mukelebe Bonventura amesema kuwa wao kama Viongozi wa Bavicha Mkoa wamejiandaa vyema kwa ajili ya Mafunzo hayo na kusema kuwa mafunzo hayo yatawaongezea uwepo wa kujiamini pamoja na utendaji wao ili kuwasaidia Watanzania wa rika mbalimbali.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top