Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAOFISA KAZI WAFAWIDHI WAKUMBUSHWA KUBORESHA UTENDAJI KAZI WAO

Katibu Mkuu, Wizara ya Kazi na Ajira, Bwana Eric Shitindi akifungua rasmi kikao cha mwaka cha siku mbili cha Maafisa Kazi Wafawidhi nchini. Kikao hicho kinafanyika kuanzia tarehe 4-5/10/2012 jijini Dar es Salaam.
……………………………………
Katibu Mkuu Wizara ya Kazi na Ajira, Bwana Eric Shitindi amewahimiza Maofisa Kazi Wafawidhi nchini kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria na kanuni za masuala ya kazi.
Bwana Shitindi aliyasema hayo leo katika hotuba yake ya ufunguzi wa kikao kazi cha Maofisa Kazi Wafawidhi kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Kazi na Ajira jijini Dar es Salaam tarehe 4/10/2012.
Bwana Shitindi aliwaeleza Maofisa Kazi Wafawidhi hao kutoka ofisi za Idara ya Kazi kote nchini kwamba wana jukumu kubwa la kujenga na kuimarisha usalama na mahusiano mema sehemu za kazi.
Kikao cha Maofisa Kazi hao kinafanyika kwa siku mbili kikiwa na lengo la kutathmini utendaji kazi wa Idara ya Kazi kwa mwaka uliopita pamoja na kujiwekea mikakati na malengo kwa mwaka ujao.
Kikao hiki kitajadili hali ya mahusiano sehemu za kazi nchini na mwelekeo wake pamoja na taarifa ya ukaguzi wa shughuli za Idara vituoni.
Akimkaribisha Katibu Mkuu wizara ya Kazi na Ajira kufungua rasmi kikao hicho, Kamishna wa Kazi, Bwana Saul Kinemela alisema kuwa vikao kazi ni mfumo waliojiwekea Maofisa Kazi kukutana kadri inavyowezekana ili kupitia, kujadili na kupanga mikakati ya utekelezaji wa kazi zao.
 Imetolewa na Ridhiwan Wema
MSEMAJI-WIZARA YA KAZI NA AJIRA
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top