****************
Na SHABANI MWINYIKAYOKA Iringa.
MAELFU ya wakazi wa Manispaa ya Iringa leo wameshiriki katika tamasha maalum la kumchangia msanii wa filamu nchini Sadik Juma Kilowoko ‘Sajuki’ Tamasha hilo limefanyika katika uwanja wa Samora na kushirikisha wasanii wengi kutoka klabu ya Bongo Movie Unity ya jijini Dar es salaam.
Awali kulikuwa na mechi ya mpira wa Miguu kati ya wasanii hao na waandishi wa habari wa mkoa wa Iringa ambapo wameweza kutoka sare ya mabao 2—2.
.
Akizungumzia tamasha hilo, mke wa Sajuki, Wastara Juma ameelezea kufurahishwa kwake na tamasha hilo na kuwashukuru wadau mbalimbali waliojitolea kulifanikisha huku pia akiwashukuru wasanii na wananchi wa mkoa wa Iringa kwa kuhudhuria katika tamasha hilo.
Naye Sajuki amewashukuru wananchi wa mkoa wa Iringa na wa Tanzania kwa ujumla kwa kufanikisha tamasha hilo kwa amani na utulivu na amemshukuru Mungu kwa kuendelea kumpa afya njema siku hadi siku na kuwaomba wadau mbalimbali waendelee kumsaidia kwani bado anahitaji matibabu.
Tamasha hilo lilipambwa na wana-Bongo movie pamoja na wasanii wa muziki wa kizazi kipya Bongo fleva na muziki wa Taarab kama vile Kitale na mfalme wa Taarab nchini na mkurugenzi wa Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf.
Kwa upande wao wananchi wa mkoa wa Iringa wameelezea kufurahishwa kwao na tamasha hilo na kuomba waandaaji waendelee kuwaletea matamasha kama hayo tamasha hilo limeandaliwa na Ibony fm, Clouds Media Group, Glory Lodge likipewa support na wasanii wa filamu kutoka Swahiliwood sambamba na watangazaji wa mkoa wa Iringa.
Na SHABANI MWINYIKAYOKA Iringa.
MAELFU ya wakazi wa Manispaa ya Iringa leo wameshiriki katika tamasha maalum la kumchangia msanii wa filamu nchini Sadik Juma Kilowoko ‘Sajuki’ Tamasha hilo limefanyika katika uwanja wa Samora na kushirikisha wasanii wengi kutoka klabu ya Bongo Movie Unity ya jijini Dar es salaam.
Awali kulikuwa na mechi ya mpira wa Miguu kati ya wasanii hao na waandishi wa habari wa mkoa wa Iringa ambapo wameweza kutoka sare ya mabao 2—2.
.
Akizungumzia tamasha hilo, mke wa Sajuki, Wastara Juma ameelezea kufurahishwa kwake na tamasha hilo na kuwashukuru wadau mbalimbali waliojitolea kulifanikisha huku pia akiwashukuru wasanii na wananchi wa mkoa wa Iringa kwa kuhudhuria katika tamasha hilo.
Naye Sajuki amewashukuru wananchi wa mkoa wa Iringa na wa Tanzania kwa ujumla kwa kufanikisha tamasha hilo kwa amani na utulivu na amemshukuru Mungu kwa kuendelea kumpa afya njema siku hadi siku na kuwaomba wadau mbalimbali waendelee kumsaidia kwani bado anahitaji matibabu.
Tamasha hilo lilipambwa na wana-Bongo movie pamoja na wasanii wa muziki wa kizazi kipya Bongo fleva na muziki wa Taarab kama vile Kitale na mfalme wa Taarab nchini na mkurugenzi wa Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf.
Kwa upande wao wananchi wa mkoa wa Iringa wameelezea kufurahishwa kwao na tamasha hilo na kuomba waandaaji waendelee kuwaletea matamasha kama hayo tamasha hilo limeandaliwa na Ibony fm, Clouds Media Group, Glory Lodge likipewa support na wasanii wa filamu kutoka Swahiliwood sambamba na watangazaji wa mkoa wa Iringa.
Post a Comment