Nyumba iliyobomoka kutokana na mvua iliyoambatana
na
upepo mkali.
ZAIDI ya familia ya 300 katika Kijiji cha Migoli,
Iringa Vijijini, hazina mahali pa kuishi kufuatia nyumba zao kubomoka na
nyingine kuezuliwa kwa upepo ulioambatana na mvua kubwa.
Mvua hiyo iliyonyesha juzi, ilianza saa 8:00 mchana ikiambatana na upepo mkali uliosambaratisha nyumba 57.
Nyumba 38 miongoni mwa hizo, zimezuliwa na nyingine 19
zimebomoka.
Diwani wa kata hiyo, Husein Kiswili. alilithibitisha habari kuhusu tukio hilo na kwamba uharibifu huo umehusisha pia miundombinu ya umeme na barabara katika eneo hilo.
““Hali ni mbaya sana, watu hawana makazi kwa sababu
nyumba nyingine zimeanguka, umeme umekatika kwa sababu nguzo zimeangushwa,”
alisema Kiswili.
Alisema mbali na nyumba za wananchi pia baadhi ya
vyumba vya madarasa ya shule ya msingi, vimeezuliwa na hivyo kusababisha
wanafunzi kukosa masomo.
Diwani huyo alisema wakazi wa kijiji hicho kwa sasa
wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.
Mbunge wa Isimani, William Lukuvi, alisema ameagiza timu ya maafa ifanye tathmini kuhusu hasara iliyowakumba wananchi hao, ili aifanyie kazi.
Lukuvi pia aliahidi kutoa mabati kwa ajili ya kuezeka
vyumba vya madarasa vilivyoezuliwa na upepo huo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk Christine
Ishengoma, alitoa kilo 750 zachakula ili kusaidiwa waathirika wa tukio
hilo.
Pia aliwataka wananchi kuwa wavuliivu na kusaidiana
katika kipindi hiki kigumu. Dk Ishengoma alisema Serikali inafanya tathimini
ili kujua kiwango cha hasara iliyopatikana kutokana na mvua hiyo.
Post a Comment