Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

HAWA NDIO WAIGIZAJI BORA WA KIUME KWA MWAKA 2012

 

1. Jacob Stephen


Mwigizaji Jacob Stephen amekuwa na mafanikio makubwa katika kazi zake ambazo zimekuwa kivutio kikubwa kwa mashabiki baada ya kubeba uhusika kama inavyo takiwa na kufanya mashabiki wake kuvutiwa na kila kazi anayoitoa.
JB mwenye umri wa miaka 52 kwa sasa ana miliki kampuni yake ya Jerusalem Film Company ambayo inafanya vizuri baada ya kuzalisha filamu zaidi ya 23.
2. Steven Kanumba

Mungu amlaze mahali pema Steven Kanumba. Bado watanzania wanakubali kazi zake ambazo alizifanya kabla hajaiyaga dunia mwanzoni mwa mwaka huu.Katika tuzo zilizoandaliwa na jarida la Babkubwa, marehemu Kanumba alishinda tuzo ya muigizaji bora wa kiume.
3. Vincent Kigosi

Kama una kumbukumbu Vincent aka Ray na Kanumba ni watu waliokuwa wakishirikiana katika kazi zao na kuna kazi walizofanya pamoja. Ray The Greatest amekubalika na jamii kwa ubora wa filamu zake za mwaka jana ikiwemo Sister Marry.
Yeye na Brandina Chagula a.k.a Johari waliamua kujiunga na kuanzisha kampuni ya kuzalisha filamu iitwayo RJ Company.
4. Hisany Muya Tino

Katika soko la filamu Tino ni actor anayekuja kwa kasi kwenye filamu za mapigano ama action. Mwaka huu ametisha na filamu yake iitwayo CID.
Hapo awali Tino alinukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari kuhusu nia yake ya kuachana na kuigiza filamu za mapenzi na kuamua kufanya za action ambazo ameonesha kuziweza.
5.Single Mtambalike

Pamoja na ukongwe, Single Mtambalike ameendelea kufanya vizuri kwenye tasnia ya filamu nchini. Kwa sasa ni mwandishi na muongozaji wa filamu. Pia ni mkurugenzi mkuu wa kampuni ya BULLS ENTERTAINMENT.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top