Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KOFI OLOMIDE AACHA HISTORIA KWA SHOW YAKE PALE LEADERS JANA


Mwanamuziki Kofii Olomide akiimba jukwaani na kundi lake katika Onesho linalofanyiki usiku huu kwenye viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar es salaam ambapo wageni waalikwa na mashabiki mbalimbali wamefurika katika viwanja hivvyo , ili waweze kushuhudia shughuli pevu ya mwanamuziki huyo nguli wa muziki Barani Afrika.

Fullshangweblog na kikozi kazi chake chote iko katika eneo la tukio ili kukumuvuzishia matukio yatakayojiri katika viwanja vya Leaders usiku huu moja kwa moja katika kukupasha habari na kukuburudisha pia.


Mmoja wa wanenguaji wa mwanamuziki Kofii Olomide akifanya vitu vyake jukwaani kama anavyoonekana katika picha.

Kofii Olomide akiimba na mmoja wa waimbaji wake Cindy.Mwanamuziki Kofii Olomide akiwa na mmoja wa waimbaji wake wa kike wakipagawisha mashabiki wa bendi hiyo waliojitokeza kwa wingi katika viwanja vya Leaders ili kushuhudia kile anachokifanya jukwaani.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Clouds Media Group akizungumza kumshukuru mwanamuziki Kofii Olomide na mashabiki waliojitokeza kwa wingi katika onesho hilo kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam.

 
Vimwana wanenguaji wa mwanamuziki Kofii Olomide wakimwaga mauno kwa kwenda mbele jukwaani katika onesho hilo.




Mwanamuziki Kofii Olomide akiwa amezungukwa na vimwana hao ambao ni wanenguajia wa bendi yake huku akiwa katikati yao kama mfalme.


Hapa ni Burudani ya mauno tu kama inavyoonekana madau.

Mashabiki mbalimbali wa mwanamuziki Kofii Olomide wakifuatilia kwa makini wakati mwanamuziki Kofii Olomide akiimba jukwaani.

Mashabiki wa mwanamziki Kofii Olomide wakishangilia kwa furaha wakati mwanamuziki Kofii Olomide akiimba jukwaani.

Mwanamuziki Kofii Olomide akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya bia ya Serengeti Bw. Steve Gannon wa pili kutoka kushoto na Mkurugenzi wa Masoko Bw. Ephraim Mafuru pamoja na wafanyakazi wengine
 
KWA PICHA ZAIDI  YA MAMBO YALIVYOKUWA KWENYE SHOW HIYO BOFYA "Read More" hapo chini



Wanamuziki wa bendi ya African Stars wakifanya vitu vyao katika Jukwaa la Tusker Canival kwenye viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar es salaam likiwa ni onesho la Utangulizi kabla ya mwanamuziki nguli wa muziki wa kiafrika Kofii Olomide ambaye anatarajiwa kupanda jukwaani muda mfupi ujao ili kuwapa burudani mashabiki wake ambao wamefurika katika viwanja hivi , ili waweze kushuhudia shughuli pevu ya mwanamuziki huyo jukwaani.
Twanga Pepeta ni raha tupu katika jukwaa la Tusker Carnival kama wanavyoonekana hapo jukwaani wakiwajibika vilivyo.Hachezi mpira wa miguu ila yuko katika kuburudisha mashabiki wake yote ikiwa ni burudani.

Mboni Masimba wa kipindi cha Mboni Show kinachorushwa na EATV akiwa na wageni wengine waalikwa katika jukwaa maalum katika onesho la Mwanamuziki Kofii Olomide linalofanyika usiku huu kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam

Kutoka kushoto ni Azda Amani kutoka SBL, Caroline Owenya na Antonina Kongoro wakipozi kwa picha.


Kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa SBL Bw. Steve Gannon, Anitha Msangi Maurice Njowoka, Agness Kiondo, Ada Amani na Nandi Mwiyombela wakipozi kwa picha.

Mkurugenzi wa Prime Time Promotion Juhayna Kusaga kulia akiwa katika picha ya pamoja na marafiki zake katika onesho hilo.

Wafanyakazi wa kampuni ya bia ya Serengeti wakijimwaga kwa kuserebuka na muziki uliokuwa ukitumbuizwa na mwanamuziki Kofii Olomide.


Wafanyakazi wa kampuni ya ndege ya Fastjet wakiwa katika onesho hilo , kutoka kushoto ni Geraldine Duwe Mkuu wa Utawala ,Prisca Simon Kitengo cha Mahusiano kwa wateja na Gladness Nahutwa Mkuu wa Mkuu wa masoko Mtandaoni.


Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti Ephraim Mafuru wa pili kutoka kushoto na Mdau Teddy Mapunda watatu kutoka kushoto wakipozi kwa picha na wafanyakazi wa kampuni ya bia ya Serengeti.

Wanamuziki wa bendi ya Diamond Misica wakifanya vitu vyao jukwaani kama wanavyoonekana.

Kutoka kulia ni Azda Amani, Agness Kiondo, Maurice Njowoka, mdau Teddy Mapunda na Caroline Owenya wakipozi kwa picha ya pamoja.

Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti Ephraim Mafuru akiwa katika picha ya pamoja na mdau Teddy Mapunda katika onesho hilo.

Kutoka kulia ni Agness Kiondo, Caroline Owenya,Azada Amani na Antonina Kongoro wakipozi kwa picha

.


Mmoja wa wanenguaji mahiri wa bendi ya Mapacha Watatu Salma Mjukuu akifanya vitu vyake jukwaani wakati bendi hiyo ilipokuwa iifanya onesho la utangulizi kabla ya mwanamuziki Kofii Olomide kupanda jukwaani kwenye viwanja vya Leaders Jijini Dar es salaam usiku huu ambapo mashabiki wanamziki kumiminika katika viwanja hivyo ili kushumshuhudia Gwiji huyo wa muziki Afrika.




Wanenguaji wa bendi ya Mapacha watatu wakio0nyesha uwezo wao katika jukwaa moja na mwanauziki Kofii Olomide hii ni nafasi nzuri kwa bendi hiyo kuonyesha kiwango chake katika muziki wa Tanzania katikati ni Jose Mara mmoja wa viongozi wa bendi hiyo


Hapa ni burudani kwa kwenda mbele kutoka Mapacha Watatu.


Kaazi kwelikweli.



Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top