Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mantra Tanazania Asa Mwaipopo (wapili kushoto) akibadirishana nyaraka za makubaliano na Mkuu wa Kituo chaUshonaji cha Utete Tailoring Mart kilichopo Songea, Mkoani Ruvuma Atnas Nyumbi (katikati) wakati wa hafla ya kukabidhi cherehani ya kisasa itakayotumika kutengeneza sare za wafanyakazi wa Kampuni ya Mantra .
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mantra
Tanazania Asa Mwaipopo (kushoto) akikabidhi cherahani ya kisasa kwa Mkuu wa
Kituo chaUshonaji cha Utete Tailoring Mart Atnas Nyumbi (kulia)ambayo itasaidia
kutengeneza sare za wafanyakazi wa Kampuni ya Mantra .
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mantra
Tanazania Asa Mwaipopo (wapili kushoto) akionyesha sare za wafanyakazi wa
kampuni hiyo zinazotengenezwa na Kituo chaUshonaji cha Utete Tailoring Mart
kilicopo Songea Mkoani Ruvuma wakati wa hafla fupi ya kukabidhi cherahani ya
kisasa kwa Mkuu wa Kituo hicho Atnas Nyumbi (kushoto)mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi Mtendaji wa
Kampuni ya Mantra Tanazania Asa Mwaipopo (kushoto) na Mkuu wa Kituo chaUshonaji
cha Utete Tailoring Mart kilichopo Songe, Mkoani Ruvuma Atnas Nyumbi (kulia)
wakitia sahihi hati za makubaliano zitakazowezesha kituo hicho kutengeneza sare
za wafanyakazi wa Kampuni ya Mantra .Picha na mpiga picha
wetu.
Na mwandishi wetu ,
Songea
KAMPUNI ya Mantra
Tanzania imeendeleza jitihada zake za kusaidia jamii inayoizunguka kwa kutoa
cherehani yakisasa inayotumia mfumo wa komputa kwa Kituo cha Ushonaji cha Utete
Tailoring Mart kilichopo mjini Songea , Mkoani Ruvuma.
Akizungumza katika
hafla fupi ya kukabidhi cherehani hiyo mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi Mtendaji wa
Kampuni ya Mantra Tanzania Asa Mwaipopo alisema kuwa kampuni yake imejizatiti
kusaida kupunguza umasikini kwa kusaidia miradi mabali mbali ya maendeleo kwenye
Mkoa huo wa Ruvuma.
Mwaipopo alisema
tayari kampuni yake imesaini hati za makubaliano na Kituo cha Ushonaji cha Utete
ambapo kituo hicho kitatengeneza sare (uniform) za wafanyakazi wa kampuni yake
hali ambayo itasaidia kujenga uwezo wa kituo hicho.
“Kampuni ya Mantra
ina nia ya kusaidia miradi mbali mbali ya maendeleo kwakutambuma umhimu wa
miradi hiyo katika kupunguza umasikini. Kwa lengo hilo, leo tunakabidhi
cherehani ya kisasa kwa kituo hichi cha Utete na tunaamini jitihada zetu
zitakuwa chachu ya maendeleo ya kituo hiki.
Mwaipopo alisema
cherehani hiyo imetolewa kwa mtindo wa mkopo wa mzunguko (Revolving Fund) na
kusema kuwa pesa itakayopatikana itasaidia kuendeleza washonaji wengine mkoani
humo.
“Atalipia kwa utaratiu
wa kazi ambazo tutakuwa tukimpa kwa makato ya taratibu. Pesa ambayo itapatikana
itasaidia kuinua washoinaji wengine. Ni matumaini yangu kuwa cherehani hii
itatumika kwa matumizi sahihi iliiweze kuka muda mrefu ,” alisema
Mwaipopo.
Maipopo alisema kuwa
kampuni yake inatakribani wafanyakazi 150 na kusema kuwa idadai hiyo itaongozeka
maradufu kufikia wafanyakazi 1500 kipindi Mradi wake wa Urani wa Mto Mkuju
utakapoanza.
“Ni matumaini yetu
kuwa sare za wafanyakazi wote hao zitatengenezwa na kituo hich cha Utete. Hii
sikazi wa mtu mmoja kwahiyo lazima kituo hiki kiaajiri washonaji wengine. Ni
matumaini yetu kuwa wananch watachangamkia fursa zitakazopatikana,”
alisema.
Naye Mkuu wa Kituo
hicho cha ushonaji cha Utete Atnas Nyumbi alisema msaada huo umekuja muda
muafaka na kuahidi kutumia cherehani hiyo vizuri ilikupata mafanikio makubwa
zaidi.
“Tunashukuru Kampuni
ya Mantra kwa kuwa na imani na kituo chetu. Tunaahidi kutumia cherehani hii
vizuri ilituweze kupata mafanikio na kusonga mbele,” alisema
Nyumbi.
Kampuni ya Mantra
Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kusadia miradi mbali mbali ya maendeleo
kwenye Mkoa wa Ruvuma ikwemo miradi ya afya, elimu, utunzaji wa mazingira pamoja
na michezo.
Post a Comment