Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS MORSI AAGIZA JESHI KUCHUKUA MAMLAKA YA POLISI NCHINI MISRI.

 






RAIS wa Misri Mohamed Morsi ameagiza jeshi nchini humo kuchukua mamlaka ya polisi kuwakamata wale wote wanaoandamana kupinga kufanyika kwa zoezi la kura ya maoni kupitisha rasimu ya katiba mpya siku ya Jumamosi, uamuzi ambao serikali inasema unaanza kutekelezwa mara moja.

Wakati uamuzi huo ukitolewa, maandamano makubwa yamepangwa kufanyika siku ya Jumanne jijini Cairo nchini Misri, yatakayoongozwa na kundi moja linalomuunga mkono rais Mohammed Morsi na lingine la upinzani.

Upinzani unasema unatumia maandamano hayo kupinga kufanyika kwa kura ya maoni kupitisha rasimu ya katiba mpya wakati wafuasi wa rais Morsi wakisema maandamano yao yatakuwa ni ya kumuunga mkono kiongozi wao.

Muungano wa vyama vya kiislamu nchini humo vinasema vinapinga wito wa upinzani wa kutaka zoezi la kura ya maoni kuahirishwa kwa kile wanachokidai kuwa huo ndio wakati wa nchi hiyo kupata katiba mpya na ni sharti zoezi hilo liendelee kama ilivyopangwa.
Marshal Mohamed Hussein Tataoui anabaki kuwa waziri wa Ulinzi, hapa ni Julay 3, 2012 jijini Cairoire.
Upinzani kwa upande wao unaona kuwa katiba hiyo mpya ikipita itawabagua pamoja na makundi ya wanawake na pia inagandamiza haki za wakiristo na wanawake.

Wiki iliyiopita, maelfu ya wapinzani waliandamana katika maeneo mbalimbali nchini humo kumshinikiza rais Mohammed Morsi kuondoa madaraka aliyojioongezea suala ambalo alisalimu amri na kuyaondoa lakini akasisitiza kuwa zoezi la kura ya maoni kuhusu katiba mpya litaendelea kama ilivyopangwa.

Jeshi nchini humo limetangaza kuwa halitaruhusu waandamanaji kuligawa tena taifa hilo na watatumia mbinu zote kuhakikisha kuwa wanalinda amani na kuepusha ghasia zilizosababisha watu saba kupoteza maisha na mamia kujeruhiwa wiki iliyopita.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top