Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Injinia Stella Manyanya akizungumza na viongozi wa Wilaya mpya ya Kalambo
alipotembelea hivi karibuni kuona jengo ambalo Mkuu wa Wilaya hiyo atalitumia
kama ofisi yake ya muda. Aliwataka viongozi pamoja na watumishi kutoweka urasimu
mbele katika utendaji kazi na badala yake kuwa kitu kimoja bila kujali cheo cha
mtu. "Kila mmoja atekeleze jukumu lake katika eneo lake na kwa kufanya hivyo
kutaifanya Wilaya hii nzuri kusonga mbele kwa kasi, kwa watumishi wa kada za
chini mnatakiwa kumuona Mkuu wa Wilaya kama rafiki na kumuona muda wowote pale
ushauri wake unapohitajika" alisema Injinia Manyanya.

Kushoto na baadhi ya
watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kalambo wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa
Rukwa Injinia Stella Manyanya alipotembelea kuona hali ya ofisi hiyo, Kulia ni
Mkuu wa Wilaya hiyo machachari ndugu Moshi Mussa Chang'a. Mkuu huyo wa Mkoa
aliwataka viongozi hao kuhakikisha suala la mipango miji bora linazingatiwa
katika kupanga miji na wilaya kwa ujumla.

Mazungumzo yakiendelea,
hata hivo Mkuu huyo wa Mkoa aliwaomba viongozi hao kuwa wavumilivu kwani
kutokana na changamoto

Mkuu wa Wilaya ya Kalambo
Ndugu Moshi Chang'a akielezea baadhi ya kero zake kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Injinia Stella Manyanya. Mkuu huyo wa Mkoa aliwapa moyo kuwa watumie uwezo wao
mdogo walionao kutatua baadhi ya kero hizo na nyingine watashirikiana
kuhakikisha zinapatiwa ufumbuzi.
Picha ya pamoja kati ya
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya na viongozi pamoja na watumishi wa
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya mpya ya Kalambo. Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya hiyo
Ndugu Moshi Chang'a.

Jengo ambalo linatumika kwa
muda kama Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kalambo.

Makazi
ya muda ya Mkuu wa Wilaya hiyo.
Na
Hamza
Temba
Afisi
Habari-Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa




Post a Comment