Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UTAMU WA DULLY KUONEKANA VIDEONI


 

Na Elizabeth John

NTOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ amaeachia video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Utamu’ amabao unafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.

Akizungumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam, Dully alisema wimbo huo kawashirikisha wakali wa muziki huo, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinum’ na Omary Faraji ‘Ommy Dimpoz’ ambao anaamini wamefanya vizuri katika wimbo huo.

“Niliamua kuwashirikisha wasanii hao kwasababu wanafanya vizuri na wanakubalika katika ‘game’, naamini uwepo wao utakuwa wa mafanikio makubwa kwangu pamoja na burudani kwa mashabiki wa muziki huo,” anasema Dully.

Anasema wimbo huo umeanza kuonekana katika vituo mbalimbali vya redio wiki hii, anawaomba mashabiki wake wampokee vizuri na kwamba wasikae mbali nay eye kuna vitu vingi ambavyo amewaandalia.

Mbali na kutaka kutoka na kibao hicho, Dully alishawahi kutamba na nyimbo zake kama Mtoto wa Kariakoo, Dhahabu na nyinginezo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika muziki wa bongo fleva.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top