Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Wanaomiliki Silaha Kinyume Cha Sheria Wapewa Siku 30 Kuzisalimisha

 


SERIKALI imetoa siku 30 kwa wananchi wanaomiliki silaha kinyume na sheria kuzisalimisha kabla hawajachukuliwa hatua za kisheria.
Kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es salaam na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Emmanuel Nchimbi wakati akizungumza na waandishi wa habari
Dkt. Nchimbi alisema kuwa na tatizo la kuzagaa na matumizi holela ya silaha zinazomilikiwa isivyo halali lichangia matukio ya uhalifu ambayo yamekuwa yakijitokeza sehemu mbalimbali nchini.Alisema kuwa kwa mfano katika mwezi Januari hadi Septemba mwaka huu kumekuwepo na matukio ya ujambazi 876 ambayo yalisababisha vifo 138 vya raia na 6 vya askari.
Aidha Dkt . Nchimbi aliongeza kuwa jumla ya mali zenye thamani ya shilingi bilioni 4.5 zilizoibiwa kwa kutumia silaha zinazomilikiwa kinyume cha sheria na zile zinazomilikiwa kisheria lakini wamiliki wake wanazitumia katika uhalifu.
Aliongeza kuwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Septemba mwaka huu jumla ya silaha 62 ziliibiwa kutoka kwa wamiliki wake halali na silaha 304 zilikamatwa katika matukio mbalimbali ya uhalifu Kufuatia hali hiyo Serikali imewaagiza watu wote wanaomiliki silaha kinyume cha Sheria kusalimisha silaha hizo katika vituo vya Polisi au wenyeviti wa vitingoji , wakuu wa mikoa na wilaya.Aidha Dk. Nchimbi alisema kuwa kwa wale ambao muda utakamailka bila kusalimisha silaha msako mkali utafanyika kuanzia tarehe 5 Januari mwakaniWaziri Nchimbi aliwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya dola kutoa taarifa zitakazosaidia kubaini uhalifu na makundi yaliyo katika jamii yetu
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright 2025 EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG | Designed By Code Nirvana
Back To Top