Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Rais ateua wenyeviti wapya Bodi za Randari na Reli


 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete(pichani), amefanya uteuzi wa Wenyeviti wapya wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Kampuni ya Reli Tanzania (TRL).


Katika uteuzi huo Rais Kikwete amemteua Prof. Joseph Msambichaka kuwa Mwenyekiti wa TPA na kutengua uteuzi wa Bwana Raphael Mollel, ambaye alikua anashikilia wadhifa huo. Prof. Msambichaka ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mbeya.


Rais Vilevile amemteua Bwana Severine M.A Kaombwe, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya TRL. Bwana Kaombwe ni Mtaalam wa Usafirishaji (East Africa Corridor Diagnostic Study for Northern and Central Corridors).


Kulingana na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Peniel Lyimo, uteuzi huu unaanza tarehe 16 Januari, 2013.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top