Katika
mahojiano na kituo cha televisheni cha Marekani CNN, Rais Mursi pia
ametabiri kwamba waasi wataweza kuipindua serikali ya Bashar al-Assad
katika vita vinavyoendelea nchini Syria.
Wizara
ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani imetupilia mbali mpango wa amani
uliopendekezwa na Assad katika hotuba yake, na kurudia wito wa kumtaka
aondoke madarakani.
Wito
kama huo wa kumtaka ajiuzulu pia ulitolewa na Umoja wa Ulaya, huku
Umoja wa Mataifa ukisema kwamba vita vinavyoendelea kwa miezi 21 nchini
Syria vimeangamiza maisha ya watu zaidi ya 60,000.
Wakati huo huo Rais Mohammed Mursi wa Misri amepokea viapo vya mawaziri wapya kumi.
Inaripotiwa
kwamba rais huyo anayo matumaini kwamba kuingizwa kwa mawaziri hao
katika serikali yake kutaimarisha imani juu ya uchumi wa Misri, huku
mazungumzo na Shirika la Fedha Ulimwenguni IMF, kuhusu mkopo
yakikaribia.
Uchumi wa Misri umekuwa ukiporomoka tangu mwaka 2011, lilipoanza vuguvugu lililomtimua madarakani rais wa zamani Hosni Mubarak.
Post a Comment