Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERIKALI KWA KUSHIRIKIANA NA WADAU KUTEKELEZA MPANGO WA MIRADI WA AFYA YA MAMA

                                                Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi

Na: Gladness Mushi Arusha
SERIKALI kwa kushirikiana na wadau inaendelea kutekeleza mpango wa miradi ya miaka mitano wa kupunguza vifo vya mama na watoto wachanga wakati wa kujifungua na walio chini ya miaka mitano ikiwa ni hatua ya kuboresha huduma ya mama na mtoto na kuokoa maisha yao.


 Hayo yameelezwa na Daktari bingwa wa akina mama na watoto wizara ya Afya na Ustawi wa jamii ,Dk Koheleth Winani, kwenye kikao cha pamoja na baadhi ya wakuu wa  mashirika mbalimbali wanaohudhuria mkutano mkuu wa kimataifa wa afya ya mama na mtoto, wanaoshirikiana na serikali kutekeleza mpango huo wa kupunguza vifo vya mama na watoto nchini walipokuwa wakitoa ufafanuzi wa maswala mbalimbali kwa wanahabari.
 Dakta Winani, amesema 75% ya watanzania wanaishi vijini ambako hawapati huduma zilizo bora wakati wa kujifungua kutokana na umbali na maeneo mengine kutopitika hasa wakati wa maska kutokana na miundo mbinu duni na kusababisha wajawazito kujifungulia majumbani au wengine kupoteza maisha wakati wakipelekwa kwenye Hospital , Vituo vya afya na Zahanati..
 Amesema kuwa mpango huo unalenga kupunguza idadi ya vifo vya wajawazito na watoto 500 mwaka 2000 hadi kufikia 19 ifikapo mwaka 2015 ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa malengo ya Milenium, na kusisitiza kuwa ushirikiano kati ya serikali na wadau hao ni muhimu kwa kuwa serikali peke yake haiwezi kutekeleza mpango huo kwa ufanisi.
 Kwa upande wake daktari Dustan Bishanga, ambae ni mkurugenzi wa mradi wa Maisha unaofadhiliwa na ,shirika la misaada la Kimarekani, USAID , kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2008 kwa thamani ya Dola milioni 40 umeboresha huduma ya afya ya mama na mtoto mchanga.
 Dakta Bishanga, amesema  mradi umetengeneza mwongozo unaotumika na wadau wengine kutekeleza mradi hiyo ,pia mradi huo unatengeneza mitaala ya kufundishia  watoa huduma kwa kushirikiana na wizara ya afya ili kutoa mafunzo  na uratibu wake katika vituo tofauti tofauti vipatavyo 250 nchini kote Tanzania bara na Zanzibar lengo ni kuboresha huduma ya mama na mtoto mchanga na kuokoa maisha
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top