Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WATU WAWILI WAJINYONGA KATIKA MATUKIO MAWILI TOFAUTI MUSOMA

 


WANAWAKE wawili katika Manispaa ya Musoma maeneo tofauti wamejinyonga huku mmoja akijinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali na mwingine akijinyonga kwa kutumia mtandio wa nguo yake
Katika tukio la kwanza mwanamke aitwaye Rudia kyango umri wa miaka 40 Mkazi wa kata ya Kigera Manispaa ya Musoma amekutwa amekufa kufuatia kujinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali na kuleta simanzi kubwa kwa familia yake.

Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia april 13 mwaka huu ambapo marehemu alijinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali na kufariki dunia na mara baada ya wakazi wa eneo hilo kufika nyumbani kwa marehemu walitoa taarifa katika kituo kidogo cha polisi kigera na polisi kuuchukua mwili wa marehemu kwa kwaajili ya uchunguzi wa kitabibu katika hospitali ya mkoa wa mara.

Wakati huo huo Mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Bhoke au mama marwa Mkazi wa Mtaa wa Ghandhi manispaa ya musoma anayekadiliwa kuwa na umri wa miaka 27 hadi 30 amejiua kwa kujinyonga kwa kutumia mtandio wa nguo yake akiwa chumbani.

Tukio hilo limetokea asubuhi leo (jana) katika mtaa wa ghandi mjini Musoma baada ya watoto wake kwenda shuleni ambapo majirani walimshuhudia na kutoa taarifa polisi.

Majirani hao waliiambia blog hii Mwanamke huyo huenda alichukua maamuzi hayo baada ya watoto wake kwenda shuleni na kubaki pekee yake nyumbani.

wamekumbana na mama huyo akiwa amejipiga kitanzi shingoni kwa kutumia mtandio wa nguo na kufariki dunia.
Umati wa wakazi wa Manispaa ya Musoma ulijaa katika eneo la tukio huku simanzi zikitawala kufuatia kifo hicho cha kujinyonga ambapo marehemu kabla ya kifo chake alikuwa anafanya kazi kwa mtu binafsi ya kuuza vinywaji baridi.

Jeshi la polisi lilifika katika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu kwaajili ya uchunguzi wa kitabibu na pia kuchunguza kubaini kilichopelekea kifo cha marehemu huyo.
Source: Shomm Binda
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top