Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MSANII WA HIP HOP LANGA AFARIKI DUNIA .... UTHIBITISHO WA KIFO CHAKE HUU HAPA





Langa Kileo (msanii wa Hip Hop Tanzania, pichani)

Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba msanii Langa amefariki dunia..


Habari zinadai kuwa , Msanii huyu alikumbwa na Malaria kali sana hali iliyopelekea kukimbizwa Hospitali ya Muhimbili jana.
UTHIBITISHO TOKA KWA AFISA UUGUZI HOSPITALI YA MUHIMBILI :
Aminiel Aligaesha ambae ni Afisa Uhusiano wa hospitali ya Taifa Muhimbili amethibitisha kwamba msanii Langa amefariki dunia June 13 2013 saa kumi na moja jioni baada ya kufikishwa hospitalini hapo toka juzi jioni ambapo kutokana na sababu za kimaadili kwenye tiba, Muhimbili hospitali hawawezi kusema rapper huyu alikua anaumwa nini bali ndugu ndio wenye mamlaka ya kufanya hivyo.
Kwenye maelezo aliyoyatoa kwa millardayo.com Aminiel amesema Marehemu Langa alipokelewa kwenye idara ya wagonjwa wa magonjwa ya dharura usiku wa kuamkia jana na kupatiwa huduma ambapo leo June 13 2013 ndio alihamishiwa kwenye chumba cha wagonjwa Mahututi na baadae kufariki dunia.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top