Imeelezwa kuwa moja kati ya neema alizopewa mwanaadamu ni umri
mrefu hivyo ni wajibu wa kila mmoja wetu kuutumia vyema uhai wake kwa kutenda
mema na kushukuru kila siku kwani hapaswi mwanaadamu kuwa aasi bali anachotakiwa
ni kumuabudu Mola wake aliyemuumba
.
Kadhi
mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji Khamis ameyasema hayo katika dua ya
kumshukuru Mwenyezi Mungu kutimiza miaka 93 ya kuzaliwa kwa Rais
Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Alhajj Aboud Jumbe Mwinyi
iliyofanyika Kiembe Samaki
.
Sheikh
Khamis Haji ametowa ukumbusho kwa kusema kuwa “ Ifanye dunia kama kwamba utaishi
milele kwa maana ya kutenda mazuri na kumuabudu Allah kama
tulivyoamrishwa katika dini pia ifanye akhera yako kama utakufa sasa kwa
maana ya kujiandaa kwa kutenda amali njema na kuomba msamaha kila siku
.
Katika
khutba yake iliyosomwa na Ustadh Moh’d Yoyota kwa niaba yake Rais Mstaafu Awamu
ya Pili Alhajj Aboud Jumbe amesema kuwa anamshukuru Mola wake
kwa umri aliyomjaalia kwani
ameshuhudia neema nyingi ambazo hazina kiima kisicho kifani,kina
wala mizani katika maisha yake na kupitia nyanja tofauti za maisha
hadi M/Mungu atakapomjaalia mwisho wa maisha yake.
Alhajj
Aboud Jumbe ameongeza kusema kuwa anamshukuru Mola wake kwa kumpa
rehema zake huruma na hisani pale alipokabidhiwa dhamana ya kuongoza
baadae kumnusuru na kumfariji na hatimae kumuongoza pale
alipoteleza mnamo asiyoyaridhia kwani majibu sahihi
ya mithani yetu wanaadamu yanasubiri siku ya malipo ambayo yatupasa tutambue
kuwa kila mmoja wetu atakutana nayo.
“Namuomba Mwenyezi Mungu kwa unyenyekevu azidi kuitakasa amali
yangu na kunipa khusni l khatima mimi pamoja na waislamu wenzangu
“
Akitowa shukurani kwa waalikwa waliohudhuria katika dua hiyo
kwa niaba ya familia ndugu Mustafa Aboud Jumbe ambae
ni mtoto wake amesema kuwa lengo la kusoma dua hii ni kukumbushana namna gani
tunatumia neema na kila mmoja vipi atautumia uhai wake na kusisitiza kuwa dua
hio ni mwenyewe baba yao aliyetowa utaratibu juu ya namna gani isomwe dua hio
“Tumekuwa tukipata masuala mengi kuhusu hali ya mzee wetu
jibu ni kwamba hajambo ila uzee tu ndio unaomsumbua, nuru ya macho
imepotea ,kusikia kumekuwa shida kidogo lakini anasikia na anazungumza na hii
shughuli yake ya leo amepanga mwenyewe”alisisitiza Mustafa
Jumbe.
Nae
Sheikh Moh’d Iddi ametowa wito kwa jamii kufanya matendo mema
kwani kuwepo kwetu ipo historia ambayo M/ Mungu amewashushia waja wake na
aliyebahatika kuishi kwa kumuabudu huyo atakuwa
amefaulu.
Post a Comment